Matukio : Kamati ya Bunge ya Huduma na Maendeleo ya Jamii Yapitisha Bajeti ya Wizara ya Habari - Wazalendo 25 Blog

Habari Mpya

Glory to Story.


Post Top Ad


31 Mar 2017

Matukio : Kamati ya Bunge ya Huduma na Maendeleo ya Jamii Yapitisha Bajeti ya Wizara ya Habari



Kamati ya Bunge ya Huduma na Maendeleo ya Jamii pamoja na Waziri, Naibu Waziri na watendaji wakuu wa Wizara na Taasisi zilizo chini yaWizara ya Habari Utamaduni Sanaa na Michezo wakijadili Bajeti ya Wizara hiyo Mjini Dodoma.

Makamu Mwenyekiti wa Kamati ya Bunge ya Huduma na Maendeleo ya Jamii Mhe. Mussa Azzan Zungu akizungumza katika kikao cha kujadili Bajeti ya Wizara ya Habari Utamaduni Sanaa na Michezo Mjini Dodoma.

Waziri wa Habari Utamaduni Sanaa na Michezo Mhe. Dkt Harrison Mwakyembe akifafanua jambo mbele ya Kamati ya Bunge ya Huduma na Maendeleo ya Jamii wakati wa kikao cha kujadili Bajeti ya Wizara ya Habari Utamaduni Sanaa na Michezo Mjini Dodoma.

Katibu Mkuu Wizara ya Habari Utamaduni Sanaa na Michezo Prof Elisante Ole Gabriel akieleza juu ya mikakati ya Wizara katika kushirikisha Sekta binafsi katika kuleta maendeleo katika Sekta za Wizara wakati wa kikao cha kuijadili Bajeti ya Wizara ya Habari Utamaduni Sanaa na Michezo Mjini Dodoma.

Baadhi ya wajumbe wa Kamati ya Bunge ya Huduma na Maendeleo ya Jamii wakifuatilia hoja mbalimbali wakati wa kikao cha kujadili Bajeti ya Wizara ya Habari Utamaduni Sanaa na Michezo Mjini Dodoma.


Picha zote na Raymond Mushumbusi WHUSM Dodoma

No comments:

Post a Comment

Post Top Ad