Kimataifa : Kikwete Akutana na Mshauri wa Trump Pembezoni mwa Mkutano wa Oslo Forum - Wazalendo 25 Blog

Glory to Story.

Habari Mpya

Friday, 12 June 2026

Kimataifa : Kikwete Akutana na Mshauri wa Trump Pembezoni mwa Mkutano wa Oslo Forum




Rais Mstaafu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete, akiwa katika picha ya pamoja na Bw. Massad Boulos, mwanadiplomasia na Mshauri Mwandamizi wa Rais Donald Trump kuhusu masuala ya Afrika, nchi za Kiarabu na Mashariki ya Kati, baada ya kufanya mazungumzo pembezoni mwa Mkutano wa Oslo Forum unaofanyika Oslo, Norway.


Mkutano huo, unaofanyika kuanzia tarehe 10 hadi 12 Juni, 2026, umewakutanisha viongozi, wanadiplomasia waandamizi na wadau wa masuala ya amani, diplomasia na usuluhishi kutoka nchi mbalimbali zenye ushawishi duniani.

No comments:

Post a Comment