Uchumi : Makamishna wa Upelelezi wa Kodi Afrika Mashariki Wakutana Dar - Wazalendo 25 Blog

Habari Mpya

Glory to Story.


Post Top Ad


28 Sept 2017

Uchumi : Makamishna wa Upelelezi wa Kodi Afrika Mashariki Wakutana Dar



Kaimu Naibu Kamishna Upelelezi wa Kodi, Eustacio Makala akisalimiana na Meneja Elimu kwa mlipa kodi, Diana Masala kabla ya kuanza kwa mkutano wa watendaji waandamizi wa Mamlaka za mapato za jumuiya ya Afrika Mashariki kwa makamishna wapelelezi kwa maswala ya kodi uliofanyika jijini Dar es Salaam leo. (Imeandaliwa na Robert Okanda Blogs)

Washiriki wa mkutano huo wakianza kwa kumtanguliza Mungu kwanza.

KAIMU Kamishna Mkuu wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA), Gerald Mwanilwa akisoma hotuba ya Kamishna Mkuu wakati wa ufunguzi wa Mkutano wa makamshina na watendaji waandamizi wa Mamlaka za mapato za jumuiya ya Afrika Mashariki kwa makamishna wapelelezi kwa maswala ya kodi uliofanyika jijini Dar es Salaam.

KAIMU Kamishna Mkuu wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA), Gerald Mwanilwa (kushoto) akibadilishana mawazo na baadhi ya watendaji waandamizi wa mamlaka hiyo wakati wa mapumziko ya Mkutano wa Mamlaka za mapato za Jumuiya ya Afrika Mashariki kwa makamishna wapelelezi kwa maswala ya kodi uliofunguliwa jijini Dar es Salaam Septemba 27 2017. Kutokea (kushoto) ni Kaimu Naibu Kamishna wa Upelelezi wa Kodi, Salim Kessi, Kaimu Naibu Kamishna Upelelezi wa Kodi, Eustacio Makala na Meneja Elimu kwa mlipa kodi, Diana Masala.

KAIMU Kamishna Mkuu wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA), Gerald Mwanilwa (katikati) akiwa katika picha ya pamoja na washiriki wa mkutano huo.

Baadhi ya washiriki wakiwa katika mkutano huo.

Baadhi ya washiriki wakiwa katika mkutano huo.

No comments:

Post a Comment

Post Top Ad