Zanzibar : Rais Dk. Shein , Mzee Mwinyi Watembelea Banda la Wizara ya mambo ya Nje - Wazalendo 25 Blog

Habari Mpya

Glory to Story.


Post Top Ad


18 Jan 2017

Zanzibar : Rais Dk. Shein , Mzee Mwinyi Watembelea Banda la Wizara ya mambo ya Nje



Rais wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Dkt. Ali Mohammed Shein akimsikiliza Afisa kutoka Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Bw. Othman Maalim Othman (kulia), wakati akitoa maelezo kuhusu majukumu ya Wizara hiyo kwa . Mwingine ni Waziri wa Biashara, Viwanda na Masoko wa Serikali ya Zanzibar, Mhe. Amina Salum Ali.

Rais wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Dkt. Ali Mohammed Shein akipatiwa maelezo ya namna ya wajasiriamali wa Tanzania watakavyoweza kufaidika kwa kutumia soko la Jumuiya ya Afrika Mashariki, kutoka kwa Bi. Vivian Rutaihwa, Afisa Biashara kutoka Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki.

Naibu Waziri (OR) wa Katiba, Sheria, Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Khamisi Juma Mwalim anbaye aliwahi kuwa mtumishi wa Wizara ya Mambo ya Nje akisaini Kitabu cha wageni katika Banda la Wizara hiyo.
Rais mstaafu wa Awamu ya pili, Alhaji Ali Hassan Mwinyi akipatiwa maelezo ya namna ya wajasiriamali wa Tanzania watakavyoweza kufaidika kwa kutumia soko la Jumuiya ya Afrika Mashariki, kutoka kwa Bi. Vivian Rutaihwa, Afisa Biashara kutoka Wizara hiyo.
Alhaji Ali Hassan Mwinyi akisaini Kitabu cha wageni katika banda la Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki.

Balozi Silima Haji Kombo, Mkurugenzi wa Idara ya Mambo ya Nje Zanzibar naye alitembelea banda la Wizara ya Mambo ya Nje.

Diwani wa Kata ya Magomeni huko Zanzibar akipata maelezo kutoka kwa Bw. Tahir Bakari, Afisa kutoka Wizara ya Mambo ya Nje kuhusu masuala mbalimbali ya utekelezaji wa Diplomasia ya Uchumi.

Waziri wa Biashara, Viwanda na Masoko wa Zanzibar, Mhe. Amina Salum Ali akitoa hotuba ya kufunga Tamsaha la Tatu la Biashara ambalo ni sehemu ya shamrashamra ya sherehe za miaka 53 ya Mapinduzi.

Mhe. Waziri akikabidhi vyeti kwa baadhi ya washiriki waTamsaha la Tatu la Biashara.

No comments:

Post a Comment

Post Top Ad