Zanzibar : Balozi Seif aongoza Maulid ya Uzawa wa Mtume Muhammad (SAW) ya Jumuiya ya Ismailia Jijini Dar es salaam. - Wazalendo 25 Blog

Habari Mpya

Glory to Story.


Post Top Ad


21 Jan 2017

Zanzibar : Balozi Seif aongoza Maulid ya Uzawa wa Mtume Muhammad (SAW) ya Jumuiya ya Ismailia Jijini Dar es salaam.






Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif Ali Iddi kulia akipokewa na Rais wa Jumuiya ya Ismailia Tanzania Bwana Amin Lakhani kwenye Maulidi ya Uzawa wa Mtume Mhammad (SAW) yaliyoandaliwa na Jumuiya hiyo hapo Upanga Mjini Dar es salaam. Kati kati yao ni Mwakilishi wa Agakhan upande wa Zanzibar Bwana Mohame Bhaloo.

Mkurugenzi wa masuala ya Taaluma na Dini ya Kiislamu na Historia wa Jumuiya ya Isimailia Tanzania Dr. Amin Rehmani akichambua masuala mbali mbali ya Dini ya Kiislamu kwenye muhadhara huo wa Maulidi.

Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif akihutubia kwenye hafla ya Maulid ya Uzawa wa Mtume Muhammad (SAW) ya Jumuiya ya Ismailia Jijini Dar es salaam.

Maustadhi wa Madrassah Shahdiliyah ya Jijini Dar wakiongoza waumini wa Dini ya Kiislamu Kwenye Mlango wa Nne wa Maulidi ya Barzanji ambapo waislamu hunyanyuka kutoa heshima ya kisimamo katika kumtukuza Kiongozi wa Dini hiyo Nabii Muhammad (SAW).

Waumini wa Dini ya Kiislamu wakipakwa mafuta mazuri ya maradhi katika kisimamo cha mlango wa Nne wa Maulid ya Barzanji ya kumtukuza Mtume Muhammad (SAW) hapo Upanga Jijini Dar es salaam.

Rais wa Jumuiya ya Ismailia Tanzania Bwana Amin Lakhani Kulia akimzawadia Mke wa Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Mama Asha Suleiman Iddi kwa ushiriki wake wa Maulidi yaliyoandaliwa na Jumuiya hiyo.

Sheikh Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam Sheikh Alhadi Mussa Salum (kulia) akipokea zawadi kutoka kwa Rais wa Jumuiya ya Ismailia Tanzania Bwana Amin Lakhani kutokana na kuthaminiwa kwa mchango wake uliofanikisha kufanyika kwa Maulidi hayo.

Mwenyekiti wa Baraza la Kiislamu Tanzania (BAKWATA) upande wa Wanawake Bibi Shamim Khan naye akipokea zawadi katika hafla hiyo ya Maulid.

Baadhi ya Waumini wa Dini ya Kiislamu waliohudhuria Maulidi ya Uzawa Mtume Muhammad (SAW) yaliyoandaliwa na Jumuiya ya Ismailia Upanga Mjini Da es salaam.

Baadhi ya Waumini wa Dini ya Kiislamu waliohudhuria Maulidi ya Uzawa Mtume Muhammad (SAW) yaliyoandaliwa na Jumuiya ya Ismailia Upanga Mjini Da es salaam.

Sheikh wa Jumuiya ya Darkhana Jamat Alfaran Dewji akisoma fatha ya kufunga hafla ya Maulidi ya Uzawa wa Mtume Muhammad (SAW) ya Jumuiya hiyo.

Viongozi Wakuu pamoja na waumini wa Dini ya Kiislamu wakiitikia dua ya kufunga rasmi kwa hafla hiyo ya Maulidi hapo Upanga Mjini Dar es salaam.

Balozi Seif pamoja na Viongozi mbali mbali wakiangalia machapisho mbali mbali vya Dini ya Kiislamu na Historia yake vilivyoandaliwa na Jumuiya Ismailia katika monyesho maalum yaliyofanyika katika hafla hiyo ya Maulid. Picha na OMPR, ZNZ.

No comments:

Post a Comment

Post Top Ad