Mafuriko : Maporomoko ya Ardhi yamshtua Mbunge - Wazalendo 25 Blog

Habari Mpya

Glory to Story.


Post Top Ad


3 May 2016

Mafuriko : Maporomoko ya Ardhi yamshtua Mbunge


Mbunge wa Jimbo la Vunjo akisalimiana na mmoja wa waathirika wa mvua kubwa iliyonyesha hivi karibuni na kusababisha kufusi kilichokuwa kando ya nyumba yake kuporomoka na kuhatarisha maisha yake katika kijiji cha Iwa ,Kirua Vunjo katika wilaya ya Moshi.
Mbunge wa jimbo la Vunjo James Mbatia akizungumza jambo mara baada ya kutembelea familia ambazo nyumba zao zimeathirika na mvua zilizonyesha hivi karibuni baada ya kuangukiwa na vifusi na kunusulika vifo.
Mbunge wa jimbo la Vunjo akitizama zoezi la uondoaji wa Vifusi vilivyo poromoka kutoka na mvua zinazoendelea kunyesha.
Sehemu ya Kifusi kilichoporomoka kando ya nyumba .
Mkazi wa kijiji cha Iwa ambaye nyumba yake iliathirika na maporomoko ya udongo yaliyotokana na mvua zinazoendelea kunyesha akimuonesha maeneo yaliyoathirika kuzunguka nyumba hiyo.
Mbunge wa jimbo la Vunjo James Mbatia akitiama sehemu ya nyuma ya nyumba hiyo ambapo pia udongo umeporomoka na kuhatarisha uwepo wa nyumba hiyo katka kijiji ch Iwa wilaya ya Moshi vijijini.
Sehemu ya Udongo ulioporomoka.
Mh akitizama nyumba nyingine iliyoathirika na maporomoko hayo ya udongo yaliyotokana na mvua zinazoendelea kunyesha.
Mbunge wa Jimbo la Vunjo ,James Mbatia akizungumza na mmoja wa wananchi katika kijiji cha Iwa  ,Kirua Vunjo katika wilaya ya Moshi ambaye nyumba yake imeathirika baada ya kuangukiwa na kifusi baada ya kuporomoka .
Mh Mbatia akitoka katika nyumba iliyoathirika na udongo ulioporomoka huku akishauri familia hizo mbili kuhama kwa muda katika nyumba zao hizo hadi pale mvua zitakapo malizika kunyesha .
Mbunge wa jimbo la Vunjo ,James Mbatia akisalimiana na wanafunzi wakati akipita kando ya barabara iliyoathirika na maporomoko ya udongo kutokana na mvua zinazoendelea kunyesha.
Mbunge Mbatia akisaidia kumbebesha udongo mmoja wa vijana waliokuwa wakijaribu kurekebisha sehemu ya barabara iliyoathirika na mvua zinazoendele kunyesha.

Na Dixon Busagaga wa Globu ya Jamii Kanda ya Kaskazini.

No comments:

Post a Comment

Post Top Ad