TEKNOLOJIA YETU : TBC YAKABIDHIWA RASMI GARI LA KISASA LA KURUSHIA MATANGAZO (OB VAN) NA SERIKALI YA CHINA - Wazalendo 25 Blog

Habari Mpya

Glory to Story.


Post Top Ad


27 Jun 2014

TEKNOLOJIA YETU : TBC YAKABIDHIWA RASMI GARI LA KISASA LA KURUSHIA MATANGAZO (OB VAN) NA SERIKALI YA CHINA


 Waziri wa Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo Dkt. Fenella Mukangara( wa pili kutoka kushoto) akikata utepe kuashiria uzinduzi rasmi wa matumizi ya Gari la kurushia matangazo la TBC, kutoka kulia ni Makamu Waziri wa Biashara wa Jamhuri ya watu wa China Li Jingzao, Makamu wa Rais wa China Li Yunchao  na wa mwisho kushoto ni Mkurugenzi wa TBC Bw. Clement Mshana
 Waziri wa Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo Dkt. Fenella Mukangara akikabidhiwa mfano wa Ufunguo wa gari la kurushia matangazo la TBC mara baada ya kuzinduliwa leo jijini Dar es Salaam.Kushoto ni Waziri wa Biashara wa Jamhuri ya Watu wa China Li Jingzao.
 Gari la kisasa la kurushia matangazo ya moja kwa moja lililokabidhiwa kwa TBC likiwa katika viwanja vya Shirika hilo Mikocheni jijini Dar es Salaam.
Kutoka kushoto ni Katibu Mkuu wa Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo Bibi. Sihaba Nkinga, Waziri wa Nchi ofisi ya Rais Utawala Bora Kapteni George Mkuchika na Mkurugenzi Mtendaji wa TBC Clement Mshana wakifuatilia mazungumzo baina ya Makumu wa Rais wa China Li Yunchao na Mwakilishi wa Startime (hawapo pichani) alipotembelea ofisi za Kampuni hiyo leo jijini Dar es Salaam.
 Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Watu wa China Li Yunchao akisalimiana na baadhi ya Wafanyakazi wa Startimes na TBC mara baada ya kuwasili katika Viwanja vya Ofisi za Shirika la Taifa la Utangazaji (TBC) alipokuwa mgeni rasmi katika hafla ya Kukabidhi na kuzindua gari la kurushia matangazo (OB Van) leo jijini Dar es Salaam.Gari hilo limetolewa kwa Msaada wa Serikali ya China.Katikati ni Waziri wa Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo wa Tanzania Dkt. Fenella Mukangara.
 Katibu Mkuu wa Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo Bibi. Sihaba Nkinga akimsikiliza kwa makini Mkurugenzi wa Idara ya Habari (MAELEZO) Bw. Assah Mwambene (katikati) wakati wa hafla ya makabidhiano na uzinduzi wa Gari la kisasa la kurushia matangazo ya moja kwa moja (OB Van) ambalo Serikali ya China ili kutoa msaada kwa Shirika la Utangazaji la Taifa (TBC). Kushoto ni Mkurugenzi wa TBC Bw. Clement Mshana.
 Msafara wa Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Watu wa China Li Yunchao ukiwasili katika Viwanja vya Ofisi za Shirika la Taifa la Utangazaji (TBC) alipotembelea kwa ajili ya hafla ya Kukabidhi na kuzindua gari la kurushia matangazo (OB Van) lililotolewa kwa Msaada wa Serikali ya China jana jijini Dar es Salaam.

No comments:

Post a Comment

Post Top Ad