TIBANYERENDA (MISA - TAN) : "TUNALAANI UKATILI NA MAOVU WANAYOFANYIWA WAANDISHI WA HABARI" - Wazalendo 25 Blog

Habari Mpya

Glory to Story.


Post Top Ad


28 Apr 2014

TIBANYERENDA (MISA - TAN) : "TUNALAANI UKATILI NA MAOVU WANAYOFANYIWA WAANDISHI WA HABARI"

DSC_0085

Picha juu na chini ni Mwenyekiti wa Taasisi ya Vyombo vya Habari Kusini mwa Afrika, Tawi la Tanzania (MISA-TAN), Bw. Mohamed Tibanyendera (wa pili kushoto) akizungumza jijini Dar es Salaam jana kuhusiana maadhimisho ya siku ya uhuru wa vyombo vya habari yatakayofanyika wiki hii duniani kote. Kushoto ni Meneja wa Maadili na Usuluhishi wa Baraza la Habari Tanzania (MCT), Allan Lawa, Afisa Habari wa kituo cha Habari cha Umoja wa Mataifa (UNIC), Bi. Usia Nkhoma Ledama (wa pili kulia) na Makamu Mwenyekiti wa Umoja wa Klabu za Waandishi wa habari Tanzania (UTPC), Jane Mihanja (kulia).(Picha na Zainul Mzige).
 DSC_0053
Na Mwandishi Wetu, Dar es Salaam
Zaidi ya washiriki 200 kutoka ndani na nje ya nchi wanatarajiwa kuhudhuria kwenye matukio ya Siku ya Uhuru wa Vyombo vya Habari Duniani, inayotarajiawa kuadhimishwa nchini hapa mnamo Mei 3, jijini Arusha, imeelezwa.
DSC_0126
Mwakilishi wa Umoja wa Mataifa ambao ni mmoja wa wadhamini wa siku ya uhuru wa vyombo vya habari duniani, Bi. Usia Nkhoma Ledama (wa pili kulia), ambaye alisisitiza kwamba uhuru wa vyombo vya habari nchini ni muhimu kusaidia nchi zinazoendela kufika malengo ya milenia.
“Sisi kama MCT tumeandaa machapisho matatu ambayo yatazinduliwa siku hiyo yanayogusia hali ya uhuru wa vyombo vya habari nchini Tanzania 2013, ripoti ya utafiti wa uvunjifu wa uhuru wa habari katika mwaka 2013, na ripoti ya ukiukwaji wa uhuru wa vyombo vya habari nchini.
“Tuna furaha kuwaambia kwamba machapisho yote haya yatapatikana siku hiyo na wote mnakaribishwa kujipatia nakala zenu,” amesema Lawa.
Akimalizia, Bw. Lawa alisema waandishi wa habari wanapaswa kufika katika ofisi za Makao Makuu ya MCT zilizopo jijini Dar es Salaam kuchukua machapisho hayo ili waweze kuyasoma kwa kina na kuweza kutambua haki zao za msingi. Alisema pia kwamba muda si mrefu, nakala za machapisho hayo zitasambazwa na kupatikana kwenye vilabu vya vyombo vya habari (Press Club) vya mikoani ili waandishi ambao wako nje ya Dar es Salaam nao waweze kunufaika na machapisho hayo.
Maadhimisho hayo yamembeba kauli mbiu ya “Uhuru wa vyombo kwa Maendeleo ya Utawala Bora”.
DSC_0144
Makamu Mwenyekiti wa Umoja wa Klabu za Waandishi wa habari Tanzania (UTPC), Jane Mihanja ambaye amesema mwandishi wa habari yoyote akizuiwa kuingia kwenye mkutano ambao ni wawazi anatakiwa kutoa taarifa katika juhudi za kuhamasisha uhuru wa vyombo vya habari nchini.
DSC_0033
Pichani juu ni chini ni baadhi ya waandishi wa habari na wadau wa tasnia hiyo waliohudhuriwa mkutano huo.

No comments:

Post a Comment

Post Top Ad