Habari na Picha za Freddy Macha
![](https://kitoto.files.wordpress.com/2017/06/8-picha-iliyoshinda-pic-by-f-macha2017.jpg)
Baadhi ya taswira zake ni : kufikiri na kuzungumza taratibu, kigugumizi, mwili mfupi, utofauti wa tambo la kichwa, vidole vya mikono na miguu, nk. Mbali na kuwanyanyapaa, jamii zetu Afrika bado hazitambui umuhimu wa kuendeleza wenye ulemavu. Mwaka huu kijana wa miaka 18, Samwel Mwanyika, mwenye “Mtindio Ubongo “ (Down Syndrome) alikuwa mshindi wa kimataifa wa upigaji picha. Balozi wetu Uingereza Mheshimiwa Asha-RoseMigiro akaeleza: “Wametoka vijana wengi kwenye nchi zilizoendelea, wengine wamemzidi umri...tena wenzetu huwa na mipango maalum ya kuwapa mbinu mbalimbali,...sasa huyu wa familia ya kawaida tu ya Kitanzania ambapo bado hatujaweka miundo mbinu kama walivyoweka huku, picha yake imeshinda...” Mwasisi wa kujitolea wa shirika la Mtindio Ubongo (Pearl of People with Down Syndrome) , Mony Teri Pettite na wazazi wake Samwel, Philip Mwanyika na Sophie Mshangama, walikutana na Balozi Migiro na kupongezwa Ijumaa iliyopita. Afisa Utawala Ubalozini, Rose Kitandula , pia alikuwepo.
Samwel Mwanyika na picha ailiyonyakua tuzo la kimataifa la Stephen Thomas, mjini London.
![](https://kitoto.files.wordpress.com/2017/06/2-balozi-migiro-akimvisha-sam-bendera-pic-by-f-macha-2017.jpg)
![](https://kitoto.files.wordpress.com/2017/06/3-rose-kitandulapenina-t-pettite-samwel-mwanyika-na-balozi-migiro-pic-by-f-macha-2017.jpg)
![](https://kitoto.files.wordpress.com/2017/06/4-picha-ya-pamoja-pic-by-fmacha-2017.jpg)
![](https://kitoto.files.wordpress.com/2017/06/5-balozi-akizungumza-na-wageni-wake-pic-by-f-macha-2017.jpg)
![](https://kitoto.files.wordpress.com/2017/06/6-balozi-na-mony-teri-pettite-pic-by-f-macha-2017.jpg)
![](https://kitoto.files.wordpress.com/2017/06/7-tuzo-ya-stpehen-thomas-pic-by-f-macha-2017.jpg)
![](https://kitoto.files.wordpress.com/2017/06/9-mama-mzazi-sophia-mshangama-akizungumza-pic-by-f-macha-2017.jpg)
No comments:
Post a Comment