Michezo : Mkolani Veterani Ndiyo Mabingwa wa 'Jembe Fm Sports Ripoti Bonanza 2017' Mwanza - Wazalendo 25 Blog

Habari Mpya

Glory to Story.


Post Top Ad


5 Jun 2017

Michezo : Mkolani Veterani Ndiyo Mabingwa wa 'Jembe Fm Sports Ripoti Bonanza 2017' Mwanza



Mkurugenzi wa Jembe Media Group Dr. Sebastian Ndege (kushoto) akiwa na mgeni Rasmi Katibu Mkuu wa Chama cha Soka mkoa wa Mwanza, Leonard Malongo (katikati) kwa pamoja wakikabidhi zawadi ya seti moja ya jezi kwa team captain wa Mkolani Veterani Fc mara baada ya kuibuka kuwa Mabingwa wa 'JEMBE FM SPORTS RIPOTI BONANZA 2017, katika uwanja wa Nyamagana. Chini ya udhamini wa Nebrix Limited wauzaji wa vifaa vya michezo na Lake Zone Tents Supply.

Si mchezo 'Miaka miwili ya changamoto hatimaye sasa nuru imeonekana'

Risala ya maadhimisho ilisomwa na Elikana Mathias.
Safu ya Meza kuu.

Mbele ya eneo la kivuli tulilolichagua kuwa jukwaa kuu.

Ni miaka miwili ya changamoto na mafanikio makubwa "Aksante sana Mwanza"

Mkurugeniz wa Jembe Media Group Dr. Sebastian Ndege akitoa shukurani kwa wananchi wa mkoa wa Mwanza wapenzi wa soka na burudani mara baada ya ushiriki wao kuweza kufanikisha tamasha la kusherehekea miaka miwili ya kipindi cha 'Sports Ripoti' kinachoruka kila siku usiku saa 3 kamili hadi 4 ikiwa ni kwa mara ya kwanza tukio hilo kufanyika, naye ameahidi kwamba maadhimisho hayo yatakuwa yakifanyika kila mwaka ambapo mwakani yataboreshwa zaidi.
Meneja wa Vipindi Redio Jembe Fm Mwanza Timothy Ngalula aka Mbaba Vc sanjari na kutoa shukurani kwa wadau Mwanza na mikoa tofauti tofauti (kupitia enternet) hapa alitambulisha safu ya watangazaji vitengo na vitengo.
Natty E eneo la tukio uwanja wa Nyamagana.

Johari Ngassa na tambo zake.......
Vanessa aka Sports Lady.
Makeke ya Babu Mkombe .

Katibu Mkuu wa Chama cha Soka mkoa wa Mwanza, Leonard Malongo ambaye alikuwa Mgeni rasmi wa Maadhimisho ya miaka miwili ya kipindi cha Sports Ripoti cha Jembe Fm akihutubia mamia ya wananchi mkoa wa Mwanza waliofika uwanja wa Nyamagana

Katibu Mkuu wa Chama cha Soka mkoa wa Mwanza, Leonard Malongo ambaye alikuwa Mgeni rasmi wa Maadhimisho ya miaka miwili ya kipindi cha Sports Ripoti cha Jembe Fm akimlisha keki mtangazaji meneja wa kipindi husika Elikana Mathias.

Katibu Mkuu wa Chama cha Soka mkoa wa Mwanza, Leonard Malongo ambaye alikuwa Mgeni rasmi wa Maadhimisho ya miaka miwili ya kipindi cha Sports Ripoti cha Jembe Fm akimlisha keki mtangazaji wa kipindi husika ambaye pia ni team captein Juma Ayoo.
Katibu Mkuu wa Chama cha Soka mkoa wa Mwanza, Leonard Malongo ambaye alikuwa Mgeni rasmi wa Maadhimisho ya miaka miwili ya kipindi cha Sports Ripoti cha Jembe Fm akimlisha keki mtangazaji wa kipindi husika 'Masamaki'

Katibu Mkuu wa Chama cha Soka mkoa wa Mwanza, Leonard Malongo ambaye alikuwa Mgeni rasmi wa Maadhimisho ya miaka miwili ya kipindi cha Sports Ripoti cha Jembe Fm akimlisha keki mtangazaji wa kipindi husika 'Sports lady' Vanessa.

Katibu Mkuu wa Chama cha Soka mkoa wa Mwanza, Leonard Malongo ambaye alikuwa Mgeni rasmi wa Maadhimisho ya miaka miwili ya kipindi cha Sports Ripoti cha Jembe Fm akimlisha keki mtangazaji wa kipindi husika Moses.

Katibu Mkuu wa Chama cha Soka mkoa wa Mwanza, Leonard Malongo ambaye alikuwa Mgeni rasmi wa Maadhimisho ya miaka miwili ya kipindi cha Sports Ripoti cha Jembe Fm akimlisha keki Mwenyekiti wa zamani MZFA Jackson Songora.

Katibu Mkuu wa Chama cha Soka mkoa wa Mwanza, Leonard Malongo ambaye alikuwa Mgeni rasmi wa Maadhimisho ya miaka miwili ya kipindi cha Sports Ripoti cha Jembe Fm akimlisha keki mchezaji wa zamani wa Pamba Fc na Yanga Africans Fumo Felician kama ishara ya shukurani.

Mshindi wa kufukuza kuku upande wa wanaume mkazi wa Igoma jijini Mwanza.

Mshindi aliyeibuka kufukuza kuku upande wa wanawake mkazi wa Mabatini jijini Mwanza.



Kwa hisani ya Heinkein ....mara baada ya vipute tulielekea kucheki fainali ya UEFA Champions League Juventus Vs Real Madrid.

Akisimulia mchezo na yatokanayo dimbani huyu ni mtangazaji wa Hit Zone majira ya saa 7 mchana hadi 10 jioni wakuitwa Babajuti.

Mtangazaji wa Sports Ripoti Juma Ayoo.

Kona ya kushoto upande wa Kaskazini Magharibu...

Wayaaaaaaa kipa wa Mjengoni Fc akiutizama mpira ....ukizama kimiani.

Macho kwenye soka.

Golikipa wa Mkolani Veterani ndiye aliyeleta shangwe kwa timu hiyo baada ya kudaka mkwaju wa kipa mwenzake wa Mjengoni Fc aka Bodaboda, ikiwa ni baada ya michomo yote kumi toka kwa wachezaji wa kila timu kushindwa kutoa mshindi.

Hureeeeeeee......

Mkolani Veterani wakisherehekea mara baada ya kuwafungwa kwa penati Mjengoni FC aka Bodaboda kutoka Sauti Malimbe jijini Mwanza




Nyuma ya kamera.

No comments:

Post a Comment

Post Top Ad