Matukio :Mashamba ya Bhangi Yateketezwa , Kasulu - Wazalendo 25 Blog

Habari Mpya

Glory to Story.


Post Top Ad


27 Mar 2017

Matukio :Mashamba ya Bhangi Yateketezwa , Kasulu


Na Rhoda Ezekiel Kigoma,

KAMATI ya ulinzi na Usalama Wilayani Kasulu imeteketeza Shamba la bhangi hekari moja iliyo kuwa ikilimwa katika hifadhi ya poli la Akiba Makere Kusini pamoja na kukamata Watuhumiwa wanne wawili wakiwa ni raia wa Burundi wakiwa wanatumiwa katika Kilimo cha hicho.

Akizungumza na waandishi wa habari Kaimu Mkuu wa wilaya ya Kasulu ambae pia ni Mkuu wa Wilaya ya Buhigwa Kanali Marko Gaguti wakati wa kuteketeza shamba hilo alisema kumekuwa na tabia ya wakulima wengi kulima bhangi pembezoni mwa mji wakichanganya na mazao Mengine suala linalopelekea watoto wengi kuharibika na uharifu kuongezeka.

Gaguti alisema baada ya kupokea taarifa kutoka kwa Wananchi kwamba kuna mtu analima bhangi jeshi la polisi kwa kushirikiana na kamati ya ulinzi na usalama ilifanya msako na kukamata shamba la Mkulima, Yotham Ngeze aliekuwa akiwatumia vibarua wanne wakiwemo warundi wawili na vijana wawili ambao walikuwa wakilima shamba hilo.

Aidha Gaguti aliwataka wakulima kuacha tabia ya kulima bhangi zao ambalo ni haramu na badala yake watumie aridhi nzuri waliyo nayo kulima mazao ya chakula kutokana na hali ya upatikanaji wa chakula ulivyo kwa sasa, na kwa atakae kutwa analima zao hilo hatua za kisheria zitachukuliwa dhidi yake Serikali inamacho mengi wataendelea kuwafuatilia popote pale .


Pia Mkuu huyo aliwataka Wakulima kuacha tabia ya kuwatumia Wahamiaji haramu katika mashamba yao hali inayo sababisha Migogoro ya Wakulima kuongezeka kutokana na ugomvi unaotokea baada ya kuwatumia vibarua hao na kuacha kuwalipa, kulikuwa na kesi nyingi za raia kutoka Burundi kuwauwa watanzania kwa kuwalipizia kisasi baada ya kuwatumia bila malipo.


"Niwaombe wakulima Muachane na tabia ya kuja kulima bhangi katika hifadhi zetu za misitu uhalifu umekuwa ukiongezeka kila siku ni kutokana na Vijana wanapo tumia madawa ya kulevya wengi wao huishia kufanya uhalifu na wengine kushindwa kuendelea na masomo hatutavumilia watoto wetu na Wananchi waendelee kuteseka tutakae Mkamata atalipa faini na kifungo pia",alisema Gaguti.

Kwa upande wake Kamanda Wa jeshi la polisi Mkoa wa Kigoma DCP Fredinandi Mtui alisema kwa Kipindi cha mwezi mmoja huu wa tatu walikamata hekari saba za bhangi na watuhumiwa nane, ambapo hekari sita ziliteketezwa katika Wilaya ya Kakonko na Hekari moja katika Wilaya ya Kasulu na jeshi la polisi linaendelea na kuwasaka wote wanao lima na kutumia bhangi ilikuweza kukomesha madawa ya kulevya.

Nae Mmiliki wa shamba la bhangi katika msitu wa hifadhi Makere Yotham Ngeze alikili kulima zao hilo na kwamba analima kwaajili ya matumizi yake binafsi na kwamba anapo tumia bhangi anajikuta anafanya kazi kubwa sana ya kulima kwa siku anaweza kulima nusu heka akiwa amwtumia zao hili.

Alisema alianza kutumia bhangi tangu mwaka 1973 akiwa katika Mashamba ya Mikonge Mkoani tabora na amekuwa akilima zao hilo liweze kumsaidia kupata bhangi kwa urahisi kutokana na mazoea aliyo jiwekea tangu akiwa kijana hawezi kuishi bila bhangi.

Nao baadhi ya vijana waliokuwa wakimlimi0a mzee huyo akiwemo Simoni Ndayahimana raia wa Burundi wamejikuta wakianza matumizi ya bhangi baada ya kulima katika shamba hilo hali inayopelekea vijana wengi kupoteza nguvu kazi kutokana na matumizi na ulimaji wa madawa ya kulevya.
Kaimu Mkuu wa wilaya ya Kasulu ambae pia ni Mkuu wa Wilaya ya Buhigwa Kanali Marko Gaguti akishiriki kuteketeza bhangi iliyokuwa imelimwa huku ikiwa imechanganywa na mazao mengine

Zoezi la kuteketeza Bhangi likindelea

Baadhi ya Watuhumiwa waliokamatwa wakiohojiwa na vyombo vya habari kufuatia kukamatwa kwa tuhuma za kulima Bhangi katika hifadhi ya poli la Akiba Makere Kusin,

No comments:

Post a Comment

Post Top Ad