Bungeni : Matukio Mbalimbali kuhusu Wizara ya Fedha na Mipango - Wazalendo 25 Blog

Habari Mpya

Glory to Story.


Post Top Ad


2 Feb 2017

Bungeni : Matukio Mbalimbali kuhusu Wizara ya Fedha na Mipango



Waziri wa Fedha na Mipango, mhe. Dkt. Philip Mpango (Mb), akifafanua baadhi ya vipengele vya Muswada wa marekebisho ya Sheria mbalimbali Namba 4 ya Mwaka 2016, kuhusu marekebisho ya Sheria ya Mikopo, Misaada na Dhamana. Muswada huo ulipitishwa kuwa Sheria na Bunge Februari Mosi, 2017.

Mwanasheria Mkuu wa Serikali, Bw. George Masaju, akihitimisha mjadala wa Muswada wa Marekebisho ya Sheria mbalimbali Namba 4 ya Mwaka 2016, uliopitishwa na wabunge kuwa Sheria Februari Mosi, 2017, Mjini Dodoma

Waziri wa Fedha na Mipango, Mhe. Dkt. Philip Mpango (Mb) na Naibu Waziri wake, Mhe. Dkt. Ashatu Kijaji (Mb), wakipitia nyaraka za Muswada wa Marekebisho ya Sheria mbalimbali Namba 4 ya Mwaka 2016, Bungeni Mjini Dodoma, Muswada ambao tayari Bunge limeupitisha kwa kishindo kuwa Sheria Februari Mosi, Mjini Dodoma.

Waziri wa Fedha na Mipango, Mhe. Dkt. Philip Mpango (Mb), akitoka nje ya ukumbi wa Bunge Mjini Dodoma baada ya kutetea na kufafanua vipengele kadhaa vya Marekebisho ya Sheria mbalimbali Namba 4 ya Mwaka 2016, husani eneo la Sheria ya Mikopo, Misaada na Dhamana, na baadaye Muswada huo kupitishwa na Bunge ili uwe Sheria, Februari Mosi, 2017, Bungeni Mjini Dodoma.

Waziri wa Fedha na Mipango, Mhe. Dkt. Philip Mpango (Mb), akimweleza jambo Naibu Waziri wa Wizara ya Nishati na Madini, Mhe. Dkt. Medard Kalemani (Mb), nje ya viwanja vya Bunge mjini Dodoma, baada ya Bunge kupitisha Muswada wa Marekebisho ya Sheria mbalimbali Namba 4 ya Mwaka 2016, Februari Mosi, 2017.(Picha na Kitengo cha Mawasiliano Serikalini-WFM)
Waziri wa Fedha na Mipango, Dkt. Philip Mpango (Mb), akimpongeza Mkurugenzi wa Idara ya Sheria wa Wizara hiyo Bi. Suzana Mkapa, Nje ya Ukumbi wa Bunge Mjini Dodoma, kwa namna alivyoshirikiana na Mwanasheria Mkuu wa Serikali Bw. George Masaju, kufanikisha Muswada wa Marekebisho ya Sheria mbalimbali Namba 4 ya Mwaka 2016, uliopitishwa na wabunge Februari Mosi, 2017.

Waziri wa Fedha na Mipango, Dkt. Philip Mpango (Mb), akifurahia jambo na maafisa waandamizi wa masuala ya Sheria na Uchumi wa Wizara yake baada ya Bunge kupitisha Muswada wa Marekebisho ya Sheria mbalimbali Namba 4 ya Mwaka 2016, uliopitishwa Februari Mosi, 2017, mjini Dodoma.

Waziri wa Fedha na Mipango, Mhe. Dkt. Philip Mpango (Mb), akiwa katika picha ya pamoja na Maafisa waandamizi wa masuala ya Sheria na Uchumi wa Wizara yake, nje ya ukumbi wa Bunge Mjini Dodoma, baada ya kupitishwa kwa marekebisho ya Sheria mbalimbali Namba 4 ya Mwaka 2016, ikiwemo Sheria ya Mikopo, Misaada na Dhamana.

Maafisa Waandamizi wa masuala ya Sheria na Uchumi wakiambatana na Mkurugenzi wa Idara ya Sheria wa Wizara ya Fedha na Mipango, Bi. Suzana Mkapa (kulia), wakiwasili kwenye viwanja vya Bunge mjini Dodoma, kusikiliza mjadala wa Bunge kuhusu Muswada wa Marekebisho ya Sheria mbalimbali Namba 4 ya Mwaka 2016, uliopitishwa na wabunge kuwa Sheria Februari Mosi, 2017.

No comments:

Post a Comment

Post Top Ad