Matukio : Taswira Mbalimbali, Mama Janeth Magufuli alivyokutana na Kufanya Mazungumzo na Mke wa Rais Wa Uturuki , Jijini Dar es Salaam - Wazalendo 25 Blog

Habari Mpya

Glory to Story.


Post Top Ad


25 Jan 2017

Matukio : Taswira Mbalimbali, Mama Janeth Magufuli alivyokutana na Kufanya Mazungumzo na Mke wa Rais Wa Uturuki , Jijini Dar es Salaam



Mke wa Rais wa Uturuki Mama Emine Erdogan akimueleza jambo Mke wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mama Janeth Magufuli Ikulu Jijini Dar es Salaam.

Mke wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mama Janeth Magufuli akimkaribisha Mke wa Rais wa Uturuki Mama Emine Erdogan Ofisini Kwake Jijini Dar es Salaam.

Mke wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mama Janeth Magufuli na Mke wa Rais wa Uturuki Mama Emine Erdogan wakifurahi na kinamama waliowalaki wakati anawasilini ofisini kwa Mke wa Rais Mama Janeth Magufuli.

Mke wa Rais wa Uturuki Mama Emine Erdogan baada ya kusaini kitabu cha wageni Ofisini Mke wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mama Janeth Magufuli.

Mke wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mama Janeth Magufuli akiwa katika picha ya pamoja na Mke wa Rais wa Uturuki Mama Emine Erdogan.




Mke wa Rais wa Uturuki Mama Emine Erdogan akiongea na Mke wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mama Janeth Magufuli ambapo amemuahidi kuendelea kushirikiana katika kuwasaidia watoto na wanawake.
Mke wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mama Janeth Magufuli akimshukuru Mke wa Rais wa Uturuki Mama Emine Erdogan kwa kufanya ziara nchini pamoja na makubaliano ya kushirikiana katika kuiendeleza jamii leo Jijini Dar es Salaam.


Mke wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mama Janeth Magufuli akimkabidhi zawadi Mke wa Rais wa Uturuki Mama Emine Erdogan leo Jijini Dar es Salaam.

Mke wa Rais wa Uturuki Mama Emine Erdogan akimkabidhi zawadi Mke wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mama Janeth Magufuli leo Jijini Dar es Salaam.

Mke wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mama Janeth Magufuli na Mke wa Rais wa Uturuki Mama Emine Erdogan wakikata utepe kuzindua jengo la zamani la King George’s V lililopo katika Jengo la makumbusho ya taifa jijini Dar es Salaam lililokarabatiwa na Shirika la Maendeleo la Uturuki (TIKA).









Mke wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mama Janeth Magufuli na Mke wa Rais wa Uturuki Mama Emine Erdogan wakitembelea maeneo mbalimbali ya historia ndani ya Jengo la makumbusho ya taifa jijini Dar es Salaam

Mke wa Rais wa Uturuki Mama Emine Erdogan akiongea na wageni alipotembelea ofisi za Shirika la Maendeleo la Uturuki (TIKA) zilizopo Masaki Jijini Dar es Salaam.

Mke wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mama Janeth Magufuli akimshukuru Mke wa Rais wa Uturuki Mama Emine Erdogan baada ya kumkabidhi viti maalum kwa ajili ya kuwasaidia watu wasiojiweza(WHEELCHAIR).

Mke wa Rais wa Uturuki Mama Emine Erdogan akikabidhi Mashine za kupumulia na kukua kwa watoto walizaliwa kabla ya muda (Njiti) Katikati ni Mke wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mama Janeth Magufuli na kulia ni Mtendaji Mkuu wa Hospitali ya Taifa ya Muhimbili Prof. Lawrence Museru, Katika Ofisi za Shirika la Maendeleo la Uturuki (TIKA).

Mke wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mama Janeth Magufuli na Mke wa Rais wa Uturuki Mama Emine Erdogan wakikata utepe kufungua Ofisi za Shirika la Maendeleo la Uturuki (TIKA) zilizopo Masaki Jijini Dar es Salaam.

Mke wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mama Janeth Magufuli na Mke wa Rais wa Uturuki Mama Emine Erdogan wakiwa katika picha ya pamoja na baadhi ya wafanyakazi wa Ofisi za Shirika la Maendeleo la Uturuki (TIKA) zilizopo Masaki Jijini Dar es Salaam.

Mke wa Rais wa Uturuki Mama Emine Erdogan akiwa amekaa katika kiti cha kabila la kigogo alipotembelea katika kijiji cha Makumbusho Kijitonyama Jijini Dar es salaam.

Mke wa Rais wa Uturuki Mama Emine Erdogan akitoka katika moja ya nyumba ya kabila la kigogo alipotembelea katika kijiji cha Makumbusho Kijitonyama Jijini Dar es salaam.



PICHA NA HASSAN SILAYO-MAELEZO.

No comments:

Post a Comment

Post Top Ad