Matukio : Mkurugenzi Mkuu wa UNEP Afanya ziara Mkoani Arusha - Wazalendo 25 Blog

Habari Mpya

Glory to Story.


Post Top Ad


25 Jan 2017

Matukio : Mkurugenzi Mkuu wa UNEP Afanya ziara Mkoani Arusha








Mkuu wa mkoa wa Arusha,Mrisho Gambo(kulia)akizungumza na Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Mazingira la Umoja wa Mataifa(UNEP),Eric Solheim katika ziara yake mkoani Arusha,Gambo ameiomba UNEP kusaidia fedha mradi wa kulinda chanzo cha maji cha Olgilai kilichopo wilayani Arumeru kinachotumika kusambaza maji jijini Arusha ambacho kimesongwa na shughuli za binadamu kikiwemo kilimo na upandaji miti ambayo sio rafiki na vyanzo vya maji.

Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Mazingira la Umoja wa Mataifa(UNEP),Eric Solheim akiwa na ujumbe wake wakifatilia mada iliyowasilishwa na Meneja wa Baraza la Mazingira Kanda ya Kaskazini(NEMC)Novatus Mushi.

Mratibu wa kitaifa wa UNEP nchini,Clara Makenya akizungumza jambo kwenye ziara hiyo,kushoto ni Katibu Tawala wa mkoa wa Arusha,Richard Kwitega na Mkuu wa wilaya ya Arusha,Gabriel Daqarro.

Mkuu wa mkoa wa Arusha,Mrisho Gambo(katikati)akiwa katika picha ya pamoja na Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Mazingira la Umoja wa Mataifa(UNEP),Eric Solheim(kushoto kwake) naa maafisa wengine wa UN pamoja na ofisi ya Mkuu wa mkoa.

Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Mazingira la Umoja wa Mataifa(UNEP),Eric Solheim(mwenye tai) akiangalia chanzo cha maji cha Mamlaka ya Maji Safi na Usafi wa Mazingiri jijini Arusha(AUWSA)eneo la Olgilai Kata ya Kiutu alikofika kuangalia uharibifu wa chanzo hicho.

No comments:

Post a Comment

Post Top Ad