
Na Dixon Busagaga Globu ya Jamii, Kanda ya Kaskazini.
Hifadhi
ya Taifa ya Serengeti kwa kushirikiana na serikali ya Korea ya
Kusini imeanza mchakato wa ujenzi wa kituo cha kimataifa cha kutunza
taarifa za mienendo ya Wanyamapori kitakachojulikana kama Serengeti
Internatinal Media Centre.
Kituo hicho kinachotarajiwa kugharimu zaidi shilingi bilioni nne kitajengwa katika Hifahi ya Taifa ya Serengeti .
Tayari
serikali ya Korea Kusini imeshatuma wajumbe wake kuja nchini
tanzania kujionea eneo kitakapojengwa kituo hicho na kukamilisha
taratibu nyingine muhimu ambapo kiongozi wa wajumbe hao Park Joosung
amesema mradi huo ni mwendelezo wa ushirikiano wa Korea Kusini na
Tanzania katika kuimarisha uhifadhi.
Akizungumza
na ujumbe huo mkuu wa hifadhi ya taifa ya serengeti Wiliam
Mwakilema amesema kituo hicho kikikamilika kitaongeza chachu utalii na
kitatoa fursa kwa wageni kuona aina nyingi zaidi za wanyama.
Naye
mratibu wa ujenzi bw Victor Ketance amesema ujenzi utaanza mwezi
october mwaka huu na unatarajiwa kumalizika baada ya miezi 14.












No comments:
Post a Comment