Utalii : Naibu Waziri, Mhandisi Makani afanya kikao na viongozi wa hifadhi ya kisiwa cha Rubondo. - Wazalendo 25 Blog

Habari Mpya

Glory to Story.


Post Top Ad


28 Jul 2016

Utalii : Naibu Waziri, Mhandisi Makani afanya kikao na viongozi wa hifadhi ya kisiwa cha Rubondo.

Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii ,Mhandisi Ramo Makani akiingia kwenye Boti kwa ajili ya kutembelea vivutio mbalimbali vya Utalii katika Hifadhi ya Taifa ya Rubondo.

Mhifadhi Mkuu wa Hifadhi ya Taifa ya Kisiwa cha Rubondo,Misana Mwishawa akimueleza jambo Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii,Mhandisi Ramo Makani wakati akitembelea vivutio mbalimbali vya utalii katika hifadhi hiyo.

Mamba ni moja ya vivutio katika Hifadhi ya Taifa ya Rubondo ambayo Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii,Mhandisi Ramo Makani alivutiwa kuwatizama.

Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii,Mhandisi Ramo Makani akitizama vivutio mbalimbali wakati akizunguka na boti maalumu katika visiwa vilivyoko Hifadhi ya Taifa ya Kisiwa cha Rubondo.

Mhifadhi Mkuu wa Hifadhi ya Taifa ya Kisiwa cha Rubondo,Missana Mwishawa akimuonesha Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii,Mhandisi Ramo Makani eneo ambalo ni makazi na mazalia ya ndege katika moja ya visiwa vilivyoko katika Hifadhi ya Taifa ya Kisiwa cha Rubondo.

Mkuu wa wilaya ya Geita,Herman Kapufi alikuwa ni mmoja wa viongozi walioongozana na Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii Mhandisi Ramo Makani kazika ziara hiyo.

Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii,Mhandisi Ramo Makani akizunbgumza jambo mara baada ya kupata maelezo mbalimbali kutoka kwa Mhifadhi Mkuu wa Hifadhi ya Taifa ya Kisiwa cha Rubondo,Misana Mwishawa

Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii,Mhandisi Ramo Makani akitia saini katika kitabu cha wageni baada ya kuwasili katika hoteli ya Asilia Lodge iliyopo ndani ya Hifadhi ya Taifa ya Kisiwa cha Rubondo.

Mkurugenzi wa Utalii na Masoko wa Shirika la Hifadhi za Taifa (TANAPA) Ibrahim Musa akizungumza wakati wa kikao kifupi cha Naibu Waziri wa Utalii na Maliasili ,Mhandisi Ramo Makani na viongozi wa Hifadhi ya Taifa ya Kisiwa cha Rubondo.

Mbunge wa Jimbo la Geita Vijijini,Joseph Kasheku (Msukuma) akizungumza wakati wa kikao hicho.

Mkuu wa wilaya ya Geita,Herman Kapufi akizungumza katika kikao hicho.

Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii ,Mhandisi Ramo Makani akizungumza na viongozi wa serikali ikiwemo kamati ya ulinzi na usalama ya mkoa wa Geita pamoja na viongozi wa Hifadhi ya Taifa ya Kisiwa cha Rubondo alipokutana nao katika Hoteli ya Asilia Lodge.

Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii,Mhandisi Ramo Makani akizungumza na mmoja wa wageni katika Hoteli ya Asilia Lodge iliyopo katika Hifadhi ya Taifa ya Kisiwa cha Rubondo.

Ugeni wa Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii,Mhandisi Ramo Makani ukipunga mikono kuaga wenyeji wao katika Hoteli ya Asilia Lodge ndani ya Hifadhi ya Taifa ya Kisiwa cha Rubondo.

Na Dixon Busagaga wa Michuzi Blog,Kanda ya Kaskazini.

No comments:

Post a Comment

Post Top Ad