Matukio : Rais Magufuli Amteua Chikawe kuwa Balozi Japan - Wazalendo 25 Blog

Habari Mpya

Glory to Story.


Post Top Ad


19 Apr 2016

Matukio : Rais Magufuli Amteua Chikawe kuwa Balozi Japan


Balozi mpya wa Tanzania nchini Japan, Mathias Chikawe./ Picha kutoka Maktaba

 Rais John Magufuli amemteua Mathias Chikawe kuwa balozi wa Tanzania nchini Japan.
Taarifa iliyotolewa leo 18 Aprili, 2016 na Katibu Mkuu Kiongozi Balozi John Kijazi, imeeleza kuwa uteuzi wa Chikawe umeanza Aprili 13, 2016.
Kabla ya kupangiwa kituo hicho cha kazi, Chikawe aliteuliwa kuwa Balozi mnamo Februari 15, 2016.
Chikawe aliwahi kuwa mbunge wa Nachingwea kati ya Mwaka 2005 na 2015, na kwa vipindi tofauti katika serikali ya awamu ya nne alikuwa Waziri wa Katiba na Sheria, Waziri wa nchi Ofisi ya Rais Utawala Bora na Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi.

No comments:

Post a Comment

Post Top Ad