Video ya Tano Bora : Nape Athibitisha Majina Matano Bora Yaliyopitishwa na Kamati Kuu - Wazalendo 25 Blog

Glory to Story.

Habari Mpya

Saturday, 11 July 2015

Video ya Tano Bora : Nape Athibitisha Majina Matano Bora Yaliyopitishwa na Kamati Kuu

 Katibu wa NEC, Itikadi na Uenezi wa CCM, Nape Nnauye akizungumza na waandishi wa habari asubuhi hii nje ya Ukumbi wa White House, Makao Makuu ya CCM Mjini Dodoma, akithibitisha taarifa iliyokuwa ikizagaa mitandaoni ya Wagombea Urais walioingia katika hatua ya tano bora, ambao aliwataja kuwa ni Waziri wa Mambo ya Nchi za Nje, Mh. Bernard Membe, Waziri wa Ujenzi, Dkt. John Magufuli, Waziri wa Katiba na Sheria, Dkt. Asha-Rose Migiro, Naibu Waziri wa Mawasiliano, Sayansi na Teknolojia, Mh. January Makamba pamoja na Balozi Amina Salum Ali. Majina hayo yanapelekwa kwenye Mkutano wa Halmashauri Kuu ya CCM Taifa kujadiliwa na kupatikana matatu yatakayopelekwa kwenye Mkutano Mkuu na kupatikana moja ambaye ndie atakuwa Mgombea Urais.

MSIKILIZE HAPA CHINI
Chanzo: Mtaa Kwa Mtaa Blog

No comments:

Post a Comment