Mazingira : Balozi wa Afrika Kusini Ashiriki Kufanya Usafi Muhimbili - Wazalendo 25 Blog

Habari Mpya

Glory to Story.


Post Top Ad


25 Jul 2015

Mazingira : Balozi wa Afrika Kusini Ashiriki Kufanya Usafi Muhimbili

 Balozi wa Afrika Kusini hapa nchini, Thami Mseleku akifanya usafi katika Wodi (A) ya Watoto iliyopo katika Taasisi ya Mifupa Muhimbili(MOI),ikiwa ni sehemu ya maadhimisho ya siku ya Kimataifa ya Nelson Mandela.
Muunganishi wa Makazi katika Umoja wa Mataifa,Alvaro Rodriguez (wa kwanza kutoka kushoto),Balozi wa Afrika Kusini nchini,Thami Mseleku (wa pili) wakiwa na baadhi ya wawakilishi wakipokea misaada kwa niaba ya walezi wengine.
Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Mifupa Muhimbili(MOI),Dkt.Othman Kiloloma akizungumza na waandishi wa habari juu ya msaada waliopokea kutoka kwa Umoja wa Mataifa,,ikiwa ni sehemu ya maadhimisho ya siku ya Kimataifa ya Nelson Mandela.
Baadhi ya wadau wakiendelea na usafi katika sehemu ya maadhimisho ya  ya siku ya Kimataifa ya Nelson Mandela. 
 Baadhi ya washiriki waliofanya usafi hospitali ya  Mhimbili Wakiwa katika picha ya pamoja. 
PICHA NA EMMANUEL MASSAKA,GLOBU YA JAMII.

No comments:

Post a Comment

Post Top Ad