AFYA YA WATOTO WETU : MAMA SALMA KIKWETE AZINDUA WIKI YA CHANJO DUNIANI, MKOANI KILIMANJARO - Wazalendo 25 Blog

Habari Mpya

Glory to Story.


Post Top Ad


30 Apr 2014

AFYA YA WATOTO WETU : MAMA SALMA KIKWETE AZINDUA WIKI YA CHANJO DUNIANI, MKOANI KILIMANJARO

Mke wa rais Mama Salma Kikwete akitoa hotuba yake wakati wa sherehe za uzinduzi wa wiki ya chanjo duniani uliofanyika katika viwanja vya mandela mjini Moshi.
Mkurugenzi
huduma za Afya toka wizara ya Afya,Dk Neema Rusibamayile akitoa neno la shukrani mara baada ya Mke wa rais,Mama Salma Kikwete kutoa hotuba yake.
Mke wa rais ,Mama Salma Kikwete akikata utepe kuashiria uzinduzi rasmi wa wiki ya chanjo duniani.
Mke wa Rais Mama Salma Kikwete akitoa chanjo ya matone kwa mtoto Ahmad Saleh kuashiria uzinduzi rasmi wa wiki ya chanjo duniani.
Mkuu wa mkoa wa Kilimanjaro Leonidas Gama akizungumza wakati wa uzinduzi wa wiki ya chanjo duniani.
Mwakilishi  mkazi wa shirika la Afya Duniani (WHO) Dk Rufaro Chatora akizungumza wakati wa sherehe za uzinduzi wa wiki ya chanjo duniani uliofanyika katika viwanja vya mandela mjini Moshi.
Baadhi ya washiriki katika uzinduzi huo kutoka Asasi mbalimbali mkoani Kilimanjaro.
Mwakilishi wa UNICEF,Sudha Sharma akizungumza wakati wa sherehe za uzinduzi wa wiki ya chanjo duniani uliofanyika katika viwanja vya mandela mjini Moshi.

No comments:

Post a Comment

Post Top Ad