RED RIBBON FASHION GALA 2012 LAKUSANYA SHILINGI MILIONI 72 - Wazalendo 25 Blog

Glory to Story.

Habari Mpya

PRINTING / GRAPHICS / DESIGN : 0784 643 633


PRINTING / GRAPHICS / DESIGN : 0676 643 633

3 Dec 2012

RED RIBBON FASHION GALA 2012 LAKUSANYA SHILINGI MILIONI 72

Omari Salisbury wa Qway International wanaosambaza vinywaji vya Belvedere Vodka akikabidhiwa cheti kwa mchango wao kutambuliwa na TMH.
Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya Mabibo Beer Wines & Spirits Ltd - Benedicta Rugemalira akitabasamu baada ya kupokea cheti kutokana na kampuni yake kutoa mchango mkubwa katika kuwezesha ufanisi wa shughuli ya kuchangisha fedha kwa ajili ya kusaidia kituo cha watoto yatima cha TMH ambapo kampuni yake Mabibo Beer Wines & Spirits ilihusika kikamilifu kunywesha wageni.
Wanamitindo Flaviana Matata na Jennifer Bash wakipita jukwaani na magauni yaliyotengenezwa na mbunifu wa kimataifa Sherri Hill wakiyanadi kwa wageni kwa ajili ya kuchangisha fedha za kusaidia kituo cha watoto yatima cha TMH.
Wanamitindo wakionyesha magauni hayo meza kuu ya wageni waalikwa akiwemo Mh. Zitto Kabwe.
Wageni waalikwa waliotia fora katika maonyesho hayo ambao walinunua magauni ya Sherri Hill kwa shilingi Milioni 4.8 Anitha (Kushoto) na Milioni 4 Alma ( wa pili kushoto) ikiwa ni mchango wao katika onyesho la Tanzania Red Ribbon Fashion Gala 2012.
Mwakilishi wa Mohammed Dewji Foundation Bw. Cosmas Mtesigwa akinunua bidhaa za mnada zilizotoka kwa mmiliki wa Kampuni ya Diamond Empowerment Fund Russel Simmons wa nchini Marekani zenye thamani ya shilingi Milioni 5 ikiwa ni mchango wa Mohammed Dewji Foundation kwa kituo cha watoto yatima cha TMH.
Mh. Zitto Kabwe akionyesha kitabu 'SUPER RICH' kilichoandikwa na Russel Simmons alichonunua kwa thamani ya Shilingi Milioni 4 kama mchango wake kwa kituo cha watoto yatima kinachoongozwa na Mwanamitindo Khadija Mwanamboka cha TMH. Kushoto ni Mwanamitindo wa Kimataifa Mtanzania anayeishi nchini Marekani aliyekuja na bidhaa hizo Flaviana Matata.
Mh. Zitto Kabwe na Chief Judge wa BSS Madam Ritha Paulsen katika Meza kuu.
Flaviana Matata na Eve Collection.
Mwakilishi wa Kampuni ya MeTL Cosmas Mtesigwa (kulia) Operation Manager wa Mo Blog Johary Kachwamba na Assistant Operation Manager Zainul Mzige nao waliokuwa miongoni mwa wageni waalikwa.
Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya Mabibo Beer Wines & Spirits Ltd Bi. Benedicta Rugemalira akiwa na binti yake mmiliki wa Eve Collection.
Mh, Zitto Kabwe sambamba na msanii Linex wakichana mistari ya wimbo wa Leka dutigite katika hafla hiyo.
Hafla hiyo ilipochanganya...... Shose Sinare naye alishindwa kujizuia na kujiunga na Mh. Zitto Kabwe na Msanii Linex katika Lekadutigite.

Mc Evance Bukuku, Nancy Sumari, Mustafa Hassanali na Asia Idarous.
Mc Abby Plaatjes na wadau.
 
 Flaviana Matata akiwaonyesha wageni baadhi ya bidhaa alizokuja nazo kutoka kwenye kampuni ya Diamond Empowerment Fund ya Russel Simmons ya nchini Marekani ambao ni mchango wa mfanyabiashara huyo wa kimataifa kwa kituo cha TMH.

No comments:

Post a Comment


PRINTING / GRAPHICS / DESIGN : 0784 643 633