MAKAMU WA RAIS DKT BILAL AWEKA JIWE LA MSINGI KITUO CHA AFYA CHA KITOMANGA, LINDI VIJIJINI - Wazalendo 25 Blog

Habari Mpya

Glory to Story.


Post Top Ad


23 Jan 2012

MAKAMU WA RAIS DKT BILAL AWEKA JIWE LA MSINGI KITUO CHA AFYA CHA KITOMANGA, LINDI VIJIJINI


Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akikata utepe kuzindua rasmi Daraja la Mingumbi lililopo Wilaya ya Kilwa, wakati akiwa katika ziara yake ya kukagua miradi ya maendeleo ya Mkoa wa Lindi jana Januari 22, 2012. Kushoto ni mkewe, Mama Zakhia Bilal (kulia) ni Mkuu wa Mkoa wa Lindi, Ludovic Mwananzila.
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akisikiliza maelezo kutoka kwa Msimamizi wa kituo cha afya cha Kitomanga, Dkt. Issa Michenje, kuhusu jengo jipya la Kituo cha afya cha Kitomanga, Lindi Vijijini, wakati akiwa katika ziara yake ya Mkoa wa Lindi jana Januari 22, 2012.

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akipunga mkono kuwasalimia wananchi baada ya kuweka Jiwe la Msingi katika jengo la Kituo cha Afya cha Kitomanga lililopo Lindi Vijijini wakati akiwa katika zaiara yake mkoa wa Lindi jana, januari 22, 2012.
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Moahammed Gharib Bilal, akizungumza na wananchi wa Kitomanga, baada ya kuzindua rasmi jengo la Kituo cha afya cha Kitomanga, Lindi Vijijini, wakati akiwa katika ziara yake ya Mkoa wa Lindi jana Januari 22, 2012.
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akiweka Jiwe la Msingi, alipozindua Daraja la Mingumbi lililopo Kilwa, wakati akiwa kwenye ziara yake ya Mkoa wa Lindi jana, Januari 22, 2012. Kulia ni Mkuu wa Mkoa wa Lindi, Ludovic Mwananzila.
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akikata utepe kuzindua rasmi Jengo jipya la Bwalo la Shule ya Sekondari ya wasichana Ilulu, iliyopo Kilwa, wakati akiwa katika ziara yake ya kukagua miradi ya maendeleo ya mkoa wa Lindi jana Januari 22, 2012. Kulia ni Mkuu wa Mkoa wa Lindi, Ludovic Mwananzila.
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akizungumza na baadhi ya wanafunzi wa Shule ya Sekondari ya wasichana ya Ilulu, baada ya kuzindua rasmi Jengo la Bwalo la shule hiyo, wakati akiwa katika ziara yake ya kukagua miradi ya maendeleo ya Mkoa wa Lindi jana Januari 22, 2012. 
Picha na Muhidin Sufiani-OMR

No comments:

Post a Comment

Post Top Ad