Michezo : Benki ya CRDB yazindua mashindano ya CRDB Bank Supa Cup 2024 - Wazalendo 25 Blog

Glory to Story.

PRINTING / GRAPHICS / DESIGN : 0784 643 633

Tuesday, 3 September 2024

demo-image

Michezo : Benki ya CRDB yazindua mashindano ya CRDB Bank Supa Cup 2024


OTMI4144
Benki ya CRDB imezindua rasmi msimu mpya wa mashindano ya mpira wa miguu na mpira wa pete yanayowahusisha wafanyakazi wake yanayotambulika kama “CRDB Bank Supa Cup 2024”, yaliyoanza kutimua vumbi siku ya Jumapili, tarehe 1 Septemba 2024, Jijini Dodoma.

Mashindano hayo yanayolenga kuongeza ari, nguvu na ushirikiano baina ya wafanyakazi wa benki hiyo, yaliyofanyika katika viwanja vya shule ya sekondari ya John Merlin. 
OTMI4135
Akizungumza wakati akifungua mashindano hayo, Afisa Mkuu wa Fedha wa Benki ya CRDB, Fredrick Nshekanabo, alisema kuwa, “Baada ya kusambaza tabasamu kwa wananchi wa Tanzania na kuvuka mipaka ya nchi kwenda nchini DR Kongo na Burundi, sasa ni zamu ya tabasamu hilo kurudi nyumbani tena na sasa ni kwa wafanyakazi.” 

Michuano hiyo  inahusisha wafanyakazi wa Benki ya CRDB kutoka matawi mbalimbali, pamoja na makao makuu wakishindana vilivyo kuwania kombe la msimu.
OTMI4191
Aidha, mashindano hayo yalienda sambasamba na programu ya kujitolea kwa wafanyakazi wa benki hiyo, ambapo siku ya Jumamosi, tarehe 31 Agosti 2024, wakiongizwa na Mkurugeni wa Rasilimali Watu, Godfrey Rutasingwa walitoa misaada ya vifaa vya kazi katika hospitali ya rufaa ya Dodoma, kuchangia damu, pamoja na kutoa chakula na vinywaji kwa wagonjwa wa hospitali hiyo.

Benki ya CRDB ilianzia programu hiyo maalumu ya wafanyakazi wake kujitolea ikilenga kusogea karibu kwa jamii wanayoihudumia. 
OTMI4029_Original
Akizungumza, Rutasingwa alisema, “Sisi kama Benki ya CRDB ni sehemu ya jamii na hatuna budi kurudi kwao kuchangia chochote kile ili kusogeza mbele maendeleo yetu. 
 
Programu hii ilizinduliwa visiwani Zanzibar mwezi uliopita na tunatarajia kuendelea kufanya hivyo katika mikoa mingine baada ya hapa Dodoma.”
OTMI4767

OTMI4615

OTMI4646

OTMI4717

OTMI4721

OTMI4747

No comments:

Post a Comment

Tuwasiliane

Name

Email *

Message *

Contact Form

Name

Email *

Message *