Miundombinu : Rais Dkt. Samia azindua Rasmi Huduma za Usafiri wa SGR kutoka Dar es Salaam - Morogoro hadi Dodoma, katika eneo la Stesheni Jijini Dar es Salaam - Wazalendo 25 Blog

Glory to Story.

Habari Mpya

PRINTING / GRAPHICS / DESIGN : 0784 643 633


PRINTING / GRAPHICS / DESIGN : 0676 643 633

1 Aug 2024

Miundombinu : Rais Dkt. Samia azindua Rasmi Huduma za Usafiri wa SGR kutoka Dar es Salaam - Morogoro hadi Dodoma, katika eneo la Stesheni Jijini Dar es Salaam


Mhe. Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan azindua Rasmi Huduma za Usafiri wa Treni ya Kisasa (SGR) kutoka Dar es Salaam - Morogoro hadi Dodoma, katika eneo la Stesheni Jijini Dar es Salaam

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akizungumza na Wananchi wa Pugu Jijini Dare es Salaam wakati akielekea Dodoma kwa Usafiri wa Treni ya Kisasa ya (SGR). Mhe. Rais Dkt. Samia amezindua Rasmi huduma za Usafiri wa Treni ya Kisasa (SGR) kuanzia eneo la Kilometa 0 Stesheni Jijini Dar es Salaam- Morogoro hadi Dodoma tarehe 01 Agosti, 2024.






Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akikata utepe kuzindua safari za Treni ya Kisasa (SGR) kuanzia eneo la Stesheni Kilometa 0 Jijini Dar es Salaam hadi Dodoma tarehe 01 Agosti, 2024.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akiwa kwenye picha na Waziri wa Uchukuzi Profesa Makame Mbarawa pamoja na Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Reli Tanzania Masanja Kadogosa mara baada ya kuwasili Stesheni ya Treni ya Kisasa (SGR) Jijini Dar es Salaam tarehe 01 Agosti, 2024.


Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akinyanyua juu Bendera na kushusha chini (Flag off) kuashiria uzinduzi rasmi wa safari za Treni ya Kisasa ya Umeme (SGR) katika eneo la Kilometa 0 Jijini Dar es Salaam hadi Dodoma tarehe 01 Agosti, 2024.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akikata utepe kuzindua jengo la Stesheni ya Treni ya Kisasa (SGR) katika eneo la Kilometa 0 Jijini Dar es Salaam tarehe 01 Agosti, 2024.

No comments:

Post a Comment


PRINTING / GRAPHICS / DESIGN : 0784 643 633