Matukio :Waziri, Jafo Aagiza Maafisa Habari Serikalini kuingia Kwenye Vikao vya Maamuzi - Wazalendo 25 Blog

Habari Mpya

Glory to Story.


Post Top Ad


18 Mar 2018

Matukio :Waziri, Jafo Aagiza Maafisa Habari Serikalini kuingia Kwenye Vikao vya Maamuzi


Na Dixon Busagaga wa Kanda ya Kaskazini.


SERIKALI imeziagiza Halmashauri kuhakikisha Maafisa Habari wanaingia katika vikao vya maamuzi ili waweze kupata na kutoa habari sahihi huku akiwatuhumu baadhi ya maafisa wa Halmashauri kuwa huendi ndio wanazuia maafisa habari kuingia katika vikao kwa lengo la kuficha baadhi ya taarifa.


Agizo hilo la serikali limetolewa na Waziri wa nchi ofisi ya Rais ,Serikaliza Mitaa(TAMISEMI) Seleman Jafo wakati wa kufunga kikao kazi cha 14 cha Maafisa Habari,Mawasiliano na Uhusiano Serikalini kilichofanyika jijini Arusha kwa muda wa siku tano.


afo pia ameziagiza Halmashauri kutenga fungu katika Bajeti zao kwa ajili ya ununuzi wa vifaa kwa ajili ya Maafisa Habari ili kusaidia katika kutekeleza majukumu yao kwa urahisi ya kuhabarisha umma shughuli mbalimbali za maendeleo zinazofanywa Serikali.


Mapema katika hotuba yake Katibu Mkuu Wizara ya Habari,Sanaa,Utamaduni na Michezo ,Susan Mlawi amesema kikao kazi hicho kimekuwa na manufaa makubwa kwa Maafisa HABAI hao na kwamba kwa sasa watakuwa na uwezo mkubwa wa kuisemea serikali.


Kikao hicho kimemalizika kwa Mgeni rasmi Waziri ofisi ya Rais ,Serikali za mitaa (TAMISEMI) Selemani Jafo kutunuku vyeti kwa Wadhamini wakuu waliofanikisha mkutano huo pamoja na viongozi wa zamani wa Chama cha Maafisa Habari,Mawasiliano na Uhusiano Serikalini (TAGCO).


Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais ,Serikali za Mitaa (TAMISEMI) Selemani Jafo akizungumza wakati wa kufunga Kikao kazi cha 14 cha Maafisa Habari,Mawasiliano na Uhusiano Serikalini kilichofanika kwa siku tano katika Ukumbi wa Mikutano ya Kimataifa (AICC) jijini Arusha.

Katibu Mkuu wa Wizara ya Habari,Sanaa ,Utamaduni na Michezo ,Susan Mlawi akizungumza wakati wa ufungaji wa Kikao Kazi cha Maafisa Habari,Mawasiliano na Uhusiano Serikali kilichofanyika jijini Arusha.

Waziri Jafo akiwa na Mkurugenzi wa Idara ya Habari ,Maelezo ,Dkt Hassan Abbas pamoja na Mwenyekiti wa Chama cha Maafisa Habari,Mawasiliano na Uhusiano Serikalini (TAGCO) Pascal Shelutete wakifuatilia hotuba ya Katibu Mkuu Wizara ya Habari ,Sanaa,Utamaduni na Michezo ,Susan Mlawa (hayupo pichani) .

Mwenyekiti wa Chama cha Maafisa Habari,Mawasiliano na Uhusiano Serikalini (TAGCO) Pascal Shelutete akizungumza wakati wa kuhitimisha siku tano za Kikao kazi cha maafisa hao kilichofanyika jijini Arusha.


Waziri wa Nchi ,Ofisi ya Rais ,Serikali za Mitaa (TAMISEMI) Selemani Jafo akikabodhi cheti kwa Mwenyekiti Mstaafu wa TAGCO ,Bw. Innocent Mungy ikiwa ni ishara ya utambuzi wa mchango wake katika chama hicho.

Waziri wa Nchi ,Ofisi ya Rais ,Serikali za Mitaa (TAMISEMI) Selemani Jafo akikabodhi cheti kwa Mmoja wa viongozi wa zamani wa TAGCO,Silvia Lupembe ambaye pia ni Meneja Mawasiliano na Uhusiano wa Chuo Kikuu cha Mzumbe ,Morogoro ikiwa ni ishara ya utambuzi wa mchango wake katika chama hicho.

Waziri wa Nchi ,Ofisi ya Rais ,Serikali za Mitaa (TAMISEMI) Selemani Jafo akikabidhi cheti Kaimu Meneja Uhusiano wa Shirika la Ugavi wa Umeme (TANESCO) Leila Muhaji kutambua mchango wa Shirika hilo katika kufanikisha kikao kazi cha maafisa Habari ,Mawasiliano na Uhusiano Serikalini kilichofanyika jijini Arusha.


Mgeni rasmi katika ufugaji wa Kikao kazi cha 14 cha Maafisa Habari,Mawasiliano na Uhusiano Serikalini ,Waziri wa Nchi ,Ofisi ya Rais,Serikali za Mitaa (TAMISEMI) Selemeni Jafo akiwa katika picha ya pamoja na Washiriki wa kikao hicho.

No comments:

Post a Comment

Post Top Ad