Afya : TDA Watua Buhangija kwa siku 2 - Wazalendo 25 Blog

Habari Mpya

Glory to Story.


Post Top Ad


14 Mar 2018

Afya : TDA Watua Buhangija kwa siku 2



Mganga Mkuu Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Shinyanga, Dr, Rashid Mfaume (wa tatu kushoto) akifungua zoezi la uchunguzi wa Afya ya Kinywa na Meno kwa watoto waliopo katika kituo cha watoto wenye mahitaji maalumu Buhangija, Mkoani Shinyanga katika kuelekea Maadhimisho ya Siku ya Afya ya Kinywa na Meno Duniani, Ambapo Kitaifa yatafanyika Machi 20, 2018,Tarime Mkoani Mara . Kuanzia kushoto ni Kiongozi wa msafara huo ambaye pia ni Daktari wa Afya ya Kinywa na Meno wa Hospitali ya Taifa Muhimbili, Dr. Arnold Mtenga, Mwalimu msaidizi wa kituo hicho, Mohamed Makana na kushoto kwa mgeni rasmi ni Daktari wa Meno Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Shinyanga, Dr. Nuru Mpuya. (PICHA ZOTE NA KHAMISI MUSSA)

Mlezi Jackson Leonard (kushoto) na Mlezi Flora Kankutebe wakifatilia jambo wakati watoto hao walipokuwa wakifanyiwa uchunguzi huku watoto wendine wakiwa katika msitari wakisubiri kufanyiwa uchunguzi


Dakt. Bingwa wa Magonjwa ya Kinywa na Meno kwa Watoto Hospitali ya Taifa Muhimbili, Dr, Conrad Mselle akimpati uji mmoja wa watoto hao huku wengine wa kiwa katika msitari wakisubiri na wao kupatiwa uji
Mwalimu msaidizi wa kituo hicho, Mohamed Makana akiwakaribisha wageni na kutoa utangulizi wa kituo hicho



Mganga Mkuu Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Shinyanga, Dr, Rashid Mfaume (wa pili kulia) mstari wa mbele katika picha ya pamoja na madaktri hao

Dakt. Bingwa wa Magonjwa ya Kinywa na Meno kwa Watoto Hospitali ya Taifa Muhimbili, Dr, Conrad Mselle akionyesha kwa mfano namna nzuri ya upigaji mswaki kwa Zephania Bahebe mmoja kati ya watoto wanaoishi katika kituo cha watoto wenye mahitaji maalumu Buhangija, Mkoani Shinyanga katika kuelekea kilele cha Maadhimisho ya Siku ya Afya ya Kinywa na Meno Duniani, Ambapo Kitaifa yatafanyika Machi 20, 2018,Tarime Mkoani Mara



Kiongozi wa msafara ambaye pia ni Daktari wa Afya ya Kinywa na Meno wa Hospitali ya Taifa Muhimbili, Dr. Arnold Mtenga akimfanyi uchunguzi wa kinywa mmoj wa watoto hao waishio kituoni hapo, Peter Tito , kulia anaye andika ni Daktari wa Hospitali ya Taifa Muhimbili, Dr. Habiba Madjapa

Kiongozi wa msafara ambaye pia ni Daktari wa Afya ya Kinywa na Meno wa Hospitali ya Taifa Muhimbili, Dr. Arnold Mtenga akizungumza n waandishi wa habari




Daktari wa Meno Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Shinyanga, Dr. Nuru Mpuya akizungumza na waandishi wa habari

No comments:

Post a Comment

Post Top Ad