Matukio : Mavunde Afungua Kongamano la Viongozi Vijana Barani Jiji Dar es Salaam - Wazalendo 25 Blog

Habari Mpya

Glory to Story.


Post Top Ad


15 Nov 2017

Matukio : Mavunde Afungua Kongamano la Viongozi Vijana Barani Jiji Dar es Salaam



Naibu Waziri Ofisi ya Waziri Mkuu, Sera , Bunge , Kazi, Vijana , ajira na Walemavu, Anthony Mavunde akizungumza wakati wa ufunguzi wa mkutano wa Viongozi Vijana Barani Afrika uliofanyika jijini Dar es Salaam leo, ambao umehudhuriwa na Vijana zaidi ya 100 kutoka Mataifa mbalimbali ,Kongamano hilo lilikuwa likijadili namna ya fursa zilizopo kwa Vijana katika kutumia rasilimali za nchi zao kama Viongozi katika kujiletea maendeleo

Mratibu wa kongamano hilo kutoka Taasisi ya The Open Society Initiative for Eastern Africa,Adam Anthony akizungumza kabl ya kumkaribisha Mgeni Rasmi kufungua kongamano hilo.

Naibu Waziri Ofisi ya Waziri Mkuu, Sera , Bunge , Kazi, Vijana , ajira na Walemavu, Anthony Mavunde akiwa meza kuu pamoja na Mratibu wa kongamano hilo kutoka Tasisi ya The Open Society Initiative for Eastern Africa,Adam Anthony na Balozi wa Uholanzi nchini Lianne Houben

Balozi wa Uholanzi nchini Lianne Houben, akitoa neno kwa vijana kama mfadhili wa kongamano hilo lililowaleta Viongozi Vijana zaidi ya 100 kutoka bara la Afrika

Msanii wa Muziki wa kughani na mshahiri maarufu barani Afrika , Mrisho Mpoto akizungumza na Waandishi wa Habari juu ya nini Vijana wanatakiwa kufanya ili waweze kuwa Viongozi bora katika Mataifa wanayotoka.

Naibu Waziri Ofisi ya Waziri Mkuu, Sera , Bunge , Kazi, Vijana , ajira na Walemavu, Anthony Mavunde , akipiga Selfier na Vijana walioshiriki Mkutano huo.


Vijana walioshiriki Mkutano wa Viongozi Vijana Barani Afrika wakifatilia mada mbalimbali zinazoendelea katika kongamano hilo

Naibu Waziri Ofisi ya Waziri Mkuu, Sera , Bunge , Kazi, Vijana , ajira na Walemavu, Anthony Mavunde akiwa katika picha ya pamoja na baadhi ya Vijana walioshiriki kongamano la Viongozi Vijana Barani Afrika

No comments:

Post a Comment

Post Top Ad