Rais wa Kwanza wa Bunge la Afrika, Getrude Mongela amesema wakati umefika kwa wanawake kuajiri na kufukuza. Alitoa kauli hiyo katika sherehe za Uzinduzi wa Jukwaa la Kuwaendeleza Wanawake Afrika (WAA) iliyofanyika kwenye hoteli ya Hyatt Regency jijini Dar es Salaam. Jukwaa hilo linasimamiwa na Taasisi ya Graca Machel. Mama Mongela alikuwa akijibu maswali ya waandishi kuhusiana na hisia zake baada ya uzinduzi na majadiliano ya Kitabu “Women Creating Wealth” ambazo ni simulizi la wanawake wajasiriamali katika bara la Afrika, waliofanikiwa na safari yao katika ujasiriamali. Alisema ingawa wakati wa Mwalimu Nyerere juhudi zilifanyika kuwawezesha wanawake, kundi hilo lilibaki kufanyakazi za kufungasha au kushona, lakini kizazi cha sasa kimeendelea kiasi ya kwamba kina uwezo wa kufanya uwekezaji na kuwa waajiri.
Rais wa Kwanza wa Bunge la Afrika, Getrude Mongela amesema wakati umefika kwa wanawake kuajiri na kufukuza. Alitoa kauli hiyo katika sherehe za Uzinduzi wa Jukwaa la Kuwaendeleza Wanawake Afrika (WAA) iliyofanyika kwenye hoteli ya Hyatt Regency jijini Dar es Salaam. Jukwaa hilo linasimamiwa na Taasisi ya Graca Machel. Mama Mongela alikuwa akijibu maswali ya waandishi kuhusiana na hisia zake baada ya uzinduzi na majadiliano ya Kitabu “Women Creating Wealth” ambazo ni simulizi la wanawake wajasiriamali katika bara la Afrika, waliofanikiwa na safari yao katika ujasiriamali. Alisema ingawa wakati wa Mwalimu Nyerere juhudi zilifanyika kuwawezesha wanawake, kundi hilo lilibaki kufanyakazi za kufungasha au kushona, lakini kizazi cha sasa kimeendelea kiasi ya kwamba kina uwezo wa kufanya uwekezaji na kuwa waajiri.

No comments:
Post a Comment