Michezo : Kagera Sugar ,JKT Ruvu watoshana nguvu - Wazalendo 25 Blog

Glory to Story.

PRINTING / GRAPHICS / DESIGN : 0784 643 633

Sunday, 9 April 2017

demo-image

Michezo : Kagera Sugar ,JKT Ruvu watoshana nguvu






Na Faustine Ruta, Bukoba
Ligi Kuu Vodacom imeendelea tena Jumamosi na katika Uwanja wa Kaitaba tukishuhudia Timu ya Kagera Sugar ikitoka sare tasa ya 0-0 dhidi ya Timu ya JKT Ruvu inayoshikilia nafasi ya mwisho kwenye msimamo wa Ligi kuu Vodacom msimu huu.
Kikosi cha Timu ya JKT Ruvu kinachonolewa na Kocha wa zamani wa Simba, Kagera Sugar, Ashanti United na sasa JKT Ruvu King Kibadeni' kilionekana kukosa mbinu kuifunga Timu ya Kagera Sugar kipindi cha pili baada ya kuonekana kuwa na nguvu kwa kuingiza wachezaji waliokuwa na kasi kubwa.
Kagera Sugar nao walikuwa wakifanya mashambulizi ya kila mara lakini hawakuweza kupata bao lolote kwenye jitihada zao zote hizo za kipindi cha kwanza na cha pili. Hadi kipindi cha pili kinalizika dakika 90 hakuna timu iliyoweza kumfunga mwenzake.
1Kikosi cha Timu ya JKT Ruvu kilichoanza kupambana na Timu ya Kagera Sugar.
2Kikosi cha Timu ya Kagera Sugar kilichoanza dhidi ya Timu ya JKT Ruvu leo kwenye Uwanja wa Kaitaba Mjini Bukoba na kutoshana nguvu kwa kutoka sare ya 0-0.
2CMchezaji wa JKT Ruvu Hassan Dirunga akiwa chini ya ulinzi wa Wachezaji wa Kagera Sugar.
2CCHassani tena akiwapa shida wachezaji wa Kagera Sugar
2DRashid Mandawa mchezaji wa zamani wa Kagera Sugar akijiandaa kuingia wakati wa kipindi cha pili cha mchezo huo kwenye Uwanja wa Kaitaba mjini Bukoba kwenye mchezo wao wa Ligi Kuu Vodacom. Picha/Habari na Faustine Ruta - Bukoba
2SMchezaji chipukizi Mbaraka Yusuph (kushoto wa Kagera Sugar akiambaa na mpira huku beki wa JKT Ruvu akimkimbiza) kipindi cha pili.
5
7Mbaraka Yusuph akilindwa na Wachezaji wa JKT Ruvu
8Dakika 90 zilikamilika na Timu zote zilitoka bila kufungana, Kagera Sugar 0-0 JKT Ruvu.
3AMchezaji hatari wa JKT Ruvu Hassan akiteta Jambo na Kocha Mkuu wa Kagera Sugar Mecky Mexime dakika 90 zilipokamilika.
DE
Kocha wa zamani wa Simba, Kagera Sugar/Ashanti United/ Abdallah King Kibadeni(kushoto) akiteteta jambo na Viongozi wa Timu ya Kagera Sugar mtanange ulipomalizika jioni hii kwenye Uwanja wa Kaitaba mjini Bukoba. Kagera Sugar imetoka sare ya 0-0 na Timu ya JKT Ruvu.

No comments:

Post a Comment

Contact Form

Name

Email *

Message *

Tuwasiliane

Name

Email *

Message *