Uchumi : AfDB Yaahidi kuendelea Kushirikiana na Tanzania Kimaendeleo - Wazalendo 25 Blog

Habari Mpya

Glory to Story.


Post Top Ad


15 Feb 2017

Uchumi : AfDB Yaahidi kuendelea Kushirikiana na Tanzania Kimaendeleo



Waziri wa Fedha na Mipango Mhe. Dkt. Philip Mpango (Mb) (kulia), akipeana mkono na Makamu wa Rais wa Benki ya Maendeleo ya Afrika (AfDB), anayeshughulikia masuala ya Nishati na Mabadiliko ya Tabianchi, Bw. Amadou Hott, (kushoto) baada ya kumalizika kwa mkutano kati yao kuhusu ahadi zilizotolewa na Benki hiyo katika kuchangia maendeleo ya Tanzania kwa njia ya ruzuku na mikopo yenye masharti nafuu, katika ukumbi wa Wizara hiyo jijini Dar es Salaam.
Waziri wa Fedha na Mipango Mhe. Dkt. Philip Mpango (Mb) (kulia), akiwa kwenye mkutano na Makamu wa Rais wa Benki ya Maendeleo ya Afrika (AfDB), anayeshughulikia masuala ya Nishati na Mabadiliko ya Tabia nchi, Bw. Amadou Hott (kushoto), ambapo Tanzania na AfdB, zimekubaliana kuendelea kushirikiana katika Nyanja mbalimbali za kiuchumi na hifadhi ya mazingira ili kukabiliana na mabadiliko ya tabia nchi, Makao Makuu ya Wizara ya Fedha na Mipango, Jijini Dar es Salaam.
Wajumbe wa mkutano wa kujadili ahadi zilizotolewa na Benki ya Maendeleo ya Afrika (AfDB), kutoka Benki hiyo na Tanzania wakifuatilia maelezo kutoka kwa Waziri wa Fedha na Mipango Mhe. Dkt. Philip Mpango (Mb), (hayupo pichani) kuhusu umuhimu wa AfDB, katika utekelezaji wa miradi mbalimbali nchini. Mkutano huo umefanyika katika ukumbi wa Wizara hiyo jijini Dar es Salaam.
Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Fedha na Mipango, Bi. Amina Khamis Shaaban (kulia), Kamishna wa Fedha za Nje wa Wizara hiyo Bw. John Rubuga (katikati) na Afisa Mwandamizi wa Wizara Bw. John Mavura wakifuatilia mjadala kuhusu ahadi zilizotolewa na Benki ya Maendeleo ya Afrika (AfDB), katika kufanikisha maendeleo ya Tanzania, katika ukumbi wa Wizara hiyo Jijini Dar es Salaam.
Waziri wa Fedha na Mipango Mhe. Dkt. Philip Mpango (Mb), akielezea kuhusu utekelezaji wa miradi ya nishati nchini alipokuwa katika kikao na Makamu wa Rais wa Benki ya Maendeleo ya Afrika (AfDB), anayeshughulikia masuala ya Nishati na Mabadiliko ya Tabia nchi, Bw. Amadou Hott, katika ukumbi wa Wizara hiyo jijini Dar es Salaam.
Makamu wa Rais wa Benki ya Maendeleo ya Afrika (AfDB), anayeshughulikia masuala ya Nishati na Mabadiliko ya Tabia nchi, Bw. Amadou Hott, akifafanua jambo katika mkutano kati yake na Waziri wa Fedha na Mipango Mhe. Dkt. Philip Mpango (Mb), katika ukumbi wa Wizara hiyo jijini Dar es Salaam.
Waziri wa Fedha na Mipango, Dkt. Philip Mpango (Mb), (Katikati) akiwa katika mkutano na ujumbe wa Benki ya Maendeleo ya Afrika (AfDB), ukiongozwa na Makamu wa Rais wa Benki hiyo anaye husika na masuala ya Nishati na Mabadiliko ya Tabia Nchi, Bw. Amadou Hott, na Ujumbe kutoka Tanzania, ambapo masuala kadhaa kuhusu uchumi, Nishati, Kilimo, Teknolojia jadidifu, yamezungumzwa ili kukuza uchumi wa nchi, Makao Makuu ya Wizara ya Fedha na Mipango, Jijini Dar es Salaam.

Waziri wa Fedha na Mipango Mhe. Dkt. Philip Mpango (Mb) na Makamu wa Rais wa Benki ya Maendeleo ya Afrika (AfDB), anayeshughulikia masuala ya Nishati na Mabadiliko ya Tabia nchi, Bw. Amadou Hott, wakiwa katika picha ya pamoja na Wajumbe wengine baada ya kumalizika kwa mkutano kuhusu ahadi zilizotolewa na Benki hiyo juu ya maendeleo ya Tanzania katika ukumbi wa Wizara hiyo jijini Dar es Salaam.

Makamu wa Rais wa Benki ya Maendeleo ya Afrika (AfDB), anayeshughulikia masuala ya Nishati na Mabadiliko ya Tabianchi, Bw. Amadou Hott (kulia), akiwasili Makao Makuu ya Wizara ya Fedha na Mipango kuonana na mwenyeji wake Waziri wa Fedha na Mipango Mhe. Dkt. Philip Mpango (Mb) jijini Dar es Salaam. (Picha na Kitengo cha Mawasiliano Serikalini-WFM)

No comments:

Post a Comment

Post Top Ad