Matukio : Majaliwa awasili Wilaya ya Longido na Kuzungumza na Watumishi - Wazalendo 25 Blog

Habari Mpya

Glory to Story.


Post Top Ad


17 Dec 2016

Matukio : Majaliwa awasili Wilaya ya Longido na Kuzungumza na Watumishi




Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akiwasalimia wananchi wa kijiji cha Londoluo waliomsimamisha akiwa njiani kutoka Loliondo kwenda Longido mkoani Arusha Desemba 16, 2016. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)


Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akisalimiana na viongozi wa wilaya ya Longido baada ya kuwasili kwenye Ofisi za Halmashauri hiyo Desemba 16, 2016.
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akizungumza na watumishi wa serikali na halmashauri ya wilaya ya Longido kwenye ukumbi wa Mwalimu Julius Kambarage Nyerere uliopo kwenye Ofisi za halmashauri hiyo Desemba 16, 2016.

Baadhi ya watumishi wa serikali na halmashauri ya wilaya ya Longido wakimsikiliza Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa wakati alipozungumza nao kwenye ukumbi wa Mwalimu Julius Kambarage Nyerere uliopo kwenye Ofisi za halmashuri hiyo Desemba 16, 2016.

Waziri wa Maliasili na Utalii, Profesa Jumanne Maghembe akiwasalimia watumishi wa halmashauri ya wilaya ya Longido kabla ya kumwalika Waziri Mkuu, Kasim Majaliwa kuzungumza nao kwenye ukumbi wa halmashauri hiyo wa Julius Kambarage Nyerere Desemba 15, 2016.

Mkuu wa Wilaya ya Longido , Daniel Chongolo, akisoma taarifa ya maendeleo ya wilaya hiyo mbele ya Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa kwenye ukumbi wa halmashuri hiyo wa Julius Kambarage Nyerere Desemba 16, 2016.

Post Top Ad