Michezo : Nitagombea Nafasi ya Katibu Mkuu RT - Wilhelm Gidabuday - Wazalendo 25 Blog

Habari Mpya

Glory to Story.


Post Top Ad


11 Oct 2016

Michezo : Nitagombea Nafasi ya Katibu Mkuu RT - Wilhelm Gidabuday

Mwanaharakati wa Michezo, Bw . Wilhelm Gidabuday.



-Ntagombea sababu ni haki yangu kikatiba katika uchaguzi ujao.

-Kwa sababu uwezo wa kuwa Mtendaji Mkuu wa taasisi hiyo ninao na kuna mifano hai ya ushirikiano nilioutoa pale nilipohitajika kufanya hivyo.

-Nitagombea iwapo Katiba halali iliyopata baraka za BMT itatumika katika uchaguzi ujao, kama katiba haitatumika sintagombea.

-Nikiwa na bahati ya kuchaguliwa nitatumia muongozo wa KATIBA na sheria za Baraza la Micheo, ama waraka wowote utakaothibitishwa na BMT au na Wizara inayohusiana na Michezo bila kuvunja sheria na Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

ILANI / MANIFEST;

-Nitajenga upya uthibiti na matumizi stahiki ya fedha za chama (Financial Discipline) ili chama kisiwe omba omba.

-Nitashawishi ujenzi wa ofisi ya chama badala ya kuomba omba pango la ofisi.

-Nitafanya kazi ya ziada kwa kushirikiana na wadhamini wa ndani na wa nje ili kujenga KAMBI YA KUDUMU ya mazoezi ili tuepuke aibu ya kutegemea Hostels ama Hoteli ambazo sharti zilipiwe kwa fedha nyingi.

-Nitakuwa namba moja kupinga kambi za nje ya nchi, mfano ile kambi ya Timu ya Madola ya 2014 pesa nyingi zilitumika kusafirisha wanariadha kwa ndege! Zile hela za serikali ziliifaidisha EMIRATE AIRLINES, badala yake ile hela ingeweza kujenga kambi ya kudumu.

-Nitahakikisha timu zinajiandaa vyema kabla ya kukabidhiwa bendera, na nitapinga timu kuchaguliwa MEZANI ama  kwa UPENDELEO! Atakayeenda ni yule aliyeshinda kwa mujibu wa Katiba na sheria za BMT.

-Nitajenga ushirikiano wa kimataifa (Sports Diplomacy na Athletics Tourism) ili kusaidiana na sekta ya Utalii kutangaza vivutio vyetu.

-Tanzania lazima ishiriki michezo yote ya kimataifa, hapatakuwa na VISINGIZIO maana fedha tutakuwa tunazisaka kwa hali na mali, na performance lazima iwe kipimo cha faida ya fedha ipatikanayo.

-Nitahakikisha RT inajipatia miradi endelevu ili tujenge "Sustainability" tuweze kujitawala wenyewe kifedha.

-Nitahakikisha viongozi wa mikoa yote Tanzania wanapokezana safari za nje badala ya mfumo HOVYO wa sasa wa kuwa na "Special Frequent Travelers" ni lazima kila kiongozi kutoka mikoa yote wapate nafasi ya "Exposure" ili warudi kujenga riadha katika mikoa yao.

-Nitahakikisha HAKI STAHIKI za wanariadha zinalindwa, kama vile CONTRACT ZA KAMPUNI ZA VIATU, MATANGAZO na BIMA ZAO ZA AFYA.

-Nikishindwa kwa mujibu wa Katiba nitafurahi na nitampongeza aliyeshinda.

-Nikishinda SINTAPAGAWA, bali nitamshukuru MUNGU na kuanza kazi ya kujenga riadha yetu.

-Kazi ya kwanza ni kuimarisha OFISI na miundombinu ya KAMBI alafu ROAD TO 2020 TOKYO OLYMPIC GAMES.

ILE FIKRA POTOFU NA YA KIFISADI ILIYOOTA MIZIZI KTK VYAMA VYA MICHEZO YA KUWEKANA MADARAKANI KINDUGU, KIKANDA NA KIRAFIKI HAINA NAFASI TENA.

By Gidabuday,
October 11th 2016.

No comments:

Post a Comment

Post Top Ad