Matukio : Jaji Lubuva aitaka Tume ya Haki za Binadamu kujifunza kwa Tume ya Uchunguzi kuimarisha Utawala Bora - Wazalendo 25 Blog

Habari Mpya

Glory to Story.


Post Top Ad


23 Oct 2016

Matukio : Jaji Lubuva aitaka Tume ya Haki za Binadamu kujifunza kwa Tume ya Uchunguzi kuimarisha Utawala Bora

Mwenyekiti wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi Jaji Mst. Damian Lubuva (kulia) akiungana kuimba wimbo wa Taifa na Mgeni Rasmi wa Maadhimisho ya Kumbukumbu ya Miaka 50 ya Kuanzishwa kwa Tume ya Kudumu ya Uchunguzi (TKU) Mhe. Waziri wa Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora Mhe. Angellah Kairuki (kushoto) na Mwenyekiti wa Tume ya Haki za Binadamu na Utawala Bora, Bahame Nyanduga, kwenye ufunguzi wa maadhimisho hayo liliyofanyika ukumbi wa Karimjee jijini Dar es Salaam.
Mwenyekiti wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi Jaji Mst. Damian Lubuva (kulia) akieleza uzoefu wake kuhusu shughuli za Tume ya Kudumu ya Uchunguzi (TKU) kwenye kongamano hilo.
Baadhi ya viongozi wa Serikali waliohudhuria Maadhimisho ya Kumbukumbu ya Miaka 50 ya Kuanzishwa kwa Tume ya Kudumu ya Uchunguzi (TKU) kwenye ukumbi wa Karimjee jijini Dar es Salaam wakiongozwa na Rais Mstafu wa Awamu ya Pili Alhaj Ali Hassan Mwinyi (wa pili kulia) wakifuatalia taarifa ya Jaji Mst. Lubuva.Wengine ni Mawaziri Wakuu Wastaafu Fredrick Sumaye (kulia), Jaji Mstaafu Joseph Warioba (wa tatu), na Mwanasheria Mkuu Mstaafu Jaji Mack Bomani na Mwenyekiti Mstaafu wa Tume ya Haki za Binadamu na Utawala Bora Jaji Kiongozi Mstaafu Amiri Manento.
Baadhi ya Wageni Waalikwa wakiwemo kutoa Ubalozi wa Sweden nchini Tanzania na Wawakilishi wa Tume ya Kudumu ya Uchunguzi za nchi za Afrika, wakifuatilia taarifa ya Jaji Mst. Lubuva.
Rais Mstaafu wa Awamu ya Pili wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Alhaj Ali Hassan Mwinyi akiwa akipokea tuzo ya Heshima ya Utawala Bora kutoka kwa Mgeni Rasmi wa Maadhimisho ya Kumbukumbu ya Miaka 50 ya Kuanzishwa kwa Tume ya Kudumu ya Uchunguzi (TKU) Mhe. Waziri wa Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora Mhe. Angellah Kairuki kwenye ukumbi wa Karimjee jijini Dar es Salaam.
Mwenyekiti wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi Jaji Mst. Damian Lubuva (katikati) akiwa amepokea Cheti cha Utambuzi wa Utumishi wake kwenye Tume ya Kudumu ya Uchunguzi (TKU) kutambua mchango wake.Kushoto ni Mwenyekiti wa Tume ya Haki za Binadamu na Utawala Bora (THBUB), Bahame Tom Nyanduga na kulia ni Katibu Mtendaji wa Tume hiyo Mary Massay.
Mwenyekiti wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi Jaji Mst. Damian Lubuva (wa tatu kulia) akiungana na kwenye picha ya pamoja na na Mgeni Rasmi wa Maadhimisho ya Kumbukumbu ya Miaka 50 ya Kuanzishwa kwa Tume ya Kudumu ya Uchunguzi (TKU) Waziri wa Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora Mhe. Angela Kairuki, Rais Mstaafu wa Awamu ya Pili Alhaj Ali Hassan Mwinyi na Viongozi wengine wa Serikali Wastaafu waliohudhuria maadhimisho hayo kwenye ukumbi wa Karimjee jijini Dar es Salaam..
Mwenyekiti wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi Jaji Mst. Damian Lubuva, akisalimiana na Rais Mstaafu wa Awamu ya Pili Alhaj Ali Hassan Mwinyi.
Mwenyekiti wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi Jaji Mst. Damian Lubuva akimueleza jambo Mgeni Rasmi wa Maadhimisho ya Kumbukumbu ya Miaka 50 ya Kuanzishwa kwa Tume ya Kudumu ya Uchunguzi (TKU) Waziri wa Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora Mhe. Angela Kairuki baada ya ufunguzi wa maadhimisho hayo.
1. Mwenyekiti wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi Jaji Mst. Damian Lubuva, akibadilisha mawazo na Wanasheria Wakuu wa Serikali Wastaafu wenzake Jaji Mst. Mark Bomani 1965-1976 na Jaji Mst. Joseph Sinde Warioba 1976 -1985.Jaji Mst. Warioba alitumikia nafasi hiyo kuanzia mwaka 1985 hadi 1993.
Mwenyekiti wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi Jaji Mst. Damian Lubuva akizungumza na kituo cha Televisheni cha ITV baada ya ufunguzi wa Maadhimisho ya Kumbukumbu ya Miaka 50 ya Kuanzishwa kwa Tume ya Kudumu ya Uchunguzi (TKU).Picha na Hussein Makame-NEC

No comments:

Post a Comment

Post Top Ad