Matukio : Madereva 10 wa Tanzania waliotekwa nchini Congo warejea , waponea tundu la sindano kuuwa - Wazalendo 25 Blog

Glory to Story.

PRINTING / GRAPHICS / DESIGN : 0784 643 633

Thursday, 22 September 2016

demo-image

Matukio : Madereva 10 wa Tanzania waliotekwa nchini Congo warejea , waponea tundu la sindano kuuwa


1
 Naibu Waziri Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Dk. Suzan Kolimba (katikati), akizungumza na madereva 10 wa Tanzania waliotekwa na watu wanaodaiwa kuwa ni waasi Jamhuri ya Demokrasia ya Conco (DRC), wakati wa hafla fupi ya kuwapokea iliyofanyika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere Dar es Salaam leo jioni. Kulia ni Balozi wa Congo nchini, Jean Mutamba na kushoto ni Mkurugenzi  Idara ya Afrika katika wizara hiyo, Balozi Samweli Shelukindo.
2
 Balozi wa Congo nchini, Jean Mutamba (kushoto), akizungumza katika hafla hiyo.
3
 Mmiliki wa Kampuni ya Simba Logistic ambayo magari yake na madereva walitekwa, Azim Dewj (kushoto), akizungumza katika hafla hiyo ya kuwapokea madereva hao.
IMG_8781
 Waandishi wa habari kutoka vyombo mbalimbali wakisubiri kuchukua taarifa za kuwapokea madereva hao.
IMG_8794
 Madereva hao wakipokelewa uwanjani hapo.
IMG_8801
 Madereva hao wakiwa chumba cha mkutano cha uwanja huo wakati wa mapokezi yao.
IMG_8840
Dereva  Mbwana Said (kulia), akielezea jinsi walivyotekwa.
IMG_8861
 Dereva Kumbuka Seleman (kulia), akisimulia jinsi alivyotoroka na kutoa taarifa ya kutekwa kwao.
IMG_8876
Dereva  Athuman Fadhili (kulia), akisimulia walivyookolewa na majeshi ya Congo na jinsi walivyojificha porini na kutembea umbali mrefu kwa kutambaa ambapo ilifika wakati waliomba bora wafe kuliko mateso waliyokuwa wakipata.
IMG_8883
 Hapa ni furaha ya kukutana na ndugu jamaa na wafanyakazi wenzao.
IMG_8888
 Picha ya pamoja na viongozi waliowapokea.
IMG_8893
 Ndugu, Jamaa, marafiki na wafanyakazi wenzao wakiwa nje ya jengo la VIP uwanjani hapo wakisubiri kuwapokea.
IMG_8900
 Mapokezi yakiendelea.
IMG_8903
Ni furaha ya kukutana na wapendwa wao.
IMG_8909
Hapa Dereva Mbwana Said akikumbatia na mjomba wake Kassim Salim katika hafla hiyo kwa Mbwana ilikuwa ni furaha na majonzi. 
IMG_8917
Mbwana Said (katikati), aamini macho yake baada ya kukutana na mke wake Mariam pamoja na mtoto wake Kauzari.

Na Dotto Mwaibale

MADEREVA 10 wa Tanzania waliotekwa na watu  wanaodhaniwa ni waasi Jamhuri ya Demokraia ya Congo (DRC) wamesema waliponea tundu la sindano kuuawa.

Kauli hiyo imetolewa na madereva hao katika hafla ya kuwapokelewa iliyofanyika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere (JNIA) Dar es Salaam leo jioni.

Akizungumza kwa niaba ya wenzake Mbwana Said alisema analishukuru jeshi la Congo kwa jitihada kubwa walioifanya kwa ajili ya kuokoa maisha yao." 

" Tunaishukuru serikali ya Congo kwa kutuokoa kwani tulikuwa katika wakati mgumu na leo kuungana tena na ndugu zetu" alisema Said.

Alisema walilazimia kutembea kwa muda mrefu huku risasi zikirindima kati ya majeshi ya serikali na waasi hao hadi walipofanikiwa kutuokowa kutoka kwenye mikono ya waasi hao. 

Naibu Waziri Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Dk. Suzan Kolimba aliishukuru serikali ya Congo kwa jitihada iliyoifanya na kufanikiwa kuwaokoa madereva hao.

Balozi wa Congo nchini Jean Mutamba aliwataka madereva hao kuacha viza na nyaraka zao ubalozini pindi wanapo safiri na kurudi ili iwe rahisi kuwatambua pale wanapopata matatizo.

"Tukio hilo limetokea kwa bahati mbaya na kutoa wito kuwa waendelee kusafiri kwa kufuata taratibu zilizopo," alisema Mutamba.

(Imeandaliwa na mtandao wa www. habari za jamii.com-simu namba 0712727062)

No comments:

Post a Comment

Tuwasiliane

Name

Email *

Message *

Contact Form

Name

Email *

Message *