Maisha : Taasisi ya THE HOPE CAMPAIGN yatoa msaada kwa watoto yatima Chamazi ,Jijini Dar - Wazalendo 25 Blog

Glory to Story.

PRINTING / GRAPHICS / DESIGN : 0784 643 633

Monday, 22 August 2016

demo-image

Maisha : Taasisi ya THE HOPE CAMPAIGN yatoa msaada kwa watoto yatima Chamazi ,Jijini Dar


IMG_0236
Mratibu wa Taasisi ya The Hope Campaign, Mpelo Kapama (kushoto), akiwaelekeza maofisa wenzake kabla ya kwenda kukabidhi msaada huo.
IMG_0246
Mizigo ikitolewa kwenye gari.
IMG_0253
Aman Issaya wa taasisi hiyo akiwa na kiroba cha sukari akielekea eneo la makabidhiano.
IMG_0256
Mratibu wa Taasisi ya The Hope Campaign, Mpelo Kapama, akiwa amebeba kiroba cha sukari wakati taasisi hiyo ilipotoa msaada wa vyakula na vifaa vya shuleni kwa Kituo cha Yatima Group Trust Fund cha Chamazi Temekie jijini Dar es Salaam leo.
IMG_0258
Vifaa hivyo viwekwa sawa kabla ya kukabidhi.
IMG_0264
Aman Issaya wa taasisi hiyo (kushoto), akimkabidhi Katibu Mkuu wa Kituo hicho, msaada huo. Kulia ni Mratibu wa Taasisi ya The Hope Campaign, Mpelo Kapama na Furaha Kapama.
IMG_0269
Furaha Kapama (kushoto), akimkabidhi msaada Katibu Mkuu wa Kituo hicho, Fred George. 


13256652_1012864148804015_371149696_n

MwezeshajiMkuu wa Kampuni hiyo, John Amigo ambaye ni mwimbaji wa nyimbo za injili akiwa katika pozi.
IMG_0273
Upendo Kapama akikabidhi msaada huo.
IMG_0276
Thomas Anzuluni akimkabidhi Katibu wa kituo hicho, Fred George msaada wa mafuta ya kula.
IMG_0280
Mwakilishi wa Taasisi ya The Hope Campaign, Stela Mpelo (kushoto), akiwakabidhi vifaa vya shule watoto Yatima wa Kituo cha Yatima Group Trust Fund cha Chamazi Temeke jijini Dar es Salaam. Kutoka kulia ni Ofisa wa taasisi hiyo, Thomas Anzuluni na Katibu wa kituo hicho, Fred George.
IMG_0285
Aman Issaya wa taasisi hiyo (kushoto), na Katibu Mkuu wa Kituo hicho wakiwa wameshika mipira iliyotolewa na taasisi hiyo kwa watoto wa kituo hicho.
IMG_0291
Hapa ni kikosi kamili cha taasisi hiyo kabla ya kukabidhi msaada huo.
IMG_0300
Ni pozi la kukata na shoka na vipeperushi mkononi.

Na Dotto Mwaibale

TAASISI ya The Hope Campaign imetoa msaada wa vyakula na vifaa vya shuleni kwa Kituo cha Yatima Group Trust Fund cha Chamazi Temeke jijini Dar es Salaam.

Akizungumza na waandishi wa habari wakati wa kukabidhi msaada huo kituoni hapo Dar es Salaam leo asubuhi , Mratibu wa Taasisi hiyo Mpelo Kapama alisema msaada huo umelenga kuwasaidia watoto hao kwa ajili ya chakula na vifaa vya kusomea.

"Taasisi yetu kupitia kwa mwezeshaji  wetu mkuu John Amigo imejijengea utamaduni wa kusaidia makundi mbalimbali yenye uhitaji kama watoto hao na kambi za ukimbizi na mara nyingi tumekuwa tukisaidia kituo hiki" alisema Kapama.

Katibu wa Kituo hicho cha Yatima, Fred George alisema ni muhimu kwa jamii kujitokeza kusaidia Yatima na kuwafariji kama ilivyofanya taasisi hiyo.

Alisema kituo hicho chenye watoto zaidi ya 150 kimekuwa na changamoto ya chakula, fedha za kuwalipa wafanyakazi pamoja na ujenzi wa uzio kwa ajili ya usalama.

(Imeandaliwa na mtandao wa www. habari za jamii.com-simu namba 0712-727062)



No comments:

Post a Comment

Contact Form

Name

Email *

Message *

Tuwasiliane

Name

Email *

Message *