Updates : Msiba wa Mtoto wa Ankal Issa Michuzi - Wazalendo 25 Blog

Habari Mpya

Glory to Story.


Post Top Ad


13 May 2016

Updates : Msiba wa Mtoto wa Ankal Issa Michuzi


Assalaam aleikum,

Familia ya Ankal Issa Michuzi iliyopatwa na msiba wa kuondokewa na Mtoto wa Ankal, Maggid Muhidin aliefariki Jumapili Mei 8, 2016 huko Durban, Afrika Kusini.

 Taarifa ya sasa ni kwamba, Ndugu zetu kule Durban wanakamilisha taratibu za kusafirisha mwili, hivyo sote tupo standby kwa hilo na naomba tufanye subira kwani hiki ni kipindi kigumu kwetu sote, na mwili ukiwasili ratiba rasmi ya mazishi itatolewa.

Msiba uko Tegeta Wazo Hill, Nyumbani kwa Mama Mzazi wa Marehemu (likiwa ni ombi maalum la Mama), na taratibu zote zinafanyika huko.

NAMNA YA KUFIKA MSIBANI
Ukitokea Tegeta Kibaoni kama unaelekea Kiwanda cha Cement Wazo, mbele mkono wako wa kulia utaona Kanisa la KKKT na ukienda mbele tena kidogo, utaona uzio wenye rangi ya njano umeandikwa Twiga Cement, unakatisha hapo upande huo huo wa kulia. ukikatisha tu utaona kuna mtaa mwingine unaingia upande wa kulia, uache na usogee mbele, utaona mtaa mwingine unaingia kulia, ingia nao huo na utakuwa umefika msibani.



Innalillah wa inna ilayhi raajiun
-AMIN.

No comments:

Post a Comment

Post Top Ad