Muziki/Mazishi : Papa Wemba azikwa Mjini Kinshasa - Wazalendo 25 Blog

Habari Mpya

Glory to Story.


Post Top Ad


6 May 2016

Muziki/Mazishi : Papa Wemba azikwa Mjini Kinshasa


Mamia kwa maelfu ya mashabiki walijitokezasiku ya Jumatano kumzika mwanamuziki mkongwe wa DRC, Papa Wemba.
Wemba, aliyezaliwa kwa jina la Jules Shungu Wembadio Pene Kikumba huko Lubefu enzi za utawala wa Wabelgiji, alianguka na kupoteza maisha wakati alipokuwa akitumbuiza jukwaani kwenye tamasha nchini Ivory Coast, April 24. Alikuwa na miaka 67.
Mwili wake uliagwa kwa siku tatu kwenye jengo la bunge la nchini hiyo mjini Kinshasa.
Makumi kwa maelfu pia walikusanyika mtaani mbele ya kanisa la Notre Dame du Congo Cathedral ambako misa ya mazishi ilifanyika. “Papa Wemba siku zote amekuwa idol wangu,” alisema JB Mpiana, kiongozi wa kundi la Wenge Musica.

No comments:

Post a Comment

Post Top Ad