Afya : GSM Foundation na MOI waanza kambi za upasuaji Bugando - Wazalendo 25 Blog

Habari Mpya

Glory to Story.


Post Top Ad


28 Apr 2016

Afya : GSM Foundation na MOI waanza kambi za upasuaji Bugando

 
Jumla ya watoto 120 wanatarajiwa kufanyiwa upasuaji katika hospitali ya Bugando jijini Mwanza, kufuatia tatizo la kichwa kikubwa walilozaliwa nalo chini ya udhamini wa taasisi ya GSM ambayo imedhamini zoezi hilo litakalofanyika katika mikoa mitano ikiwa ni awamu ya kwanza kati ya nne zinazotarajiwa kufanyika tanzania nzima.

Akiongea na waandishi wa habari katika uzinduzi wa zoezi hilo linalojumuisha madaktari Bingwa 10 kutoka Taasisi ya mifupa na Upasuaji MOI, Mkurugenzi Mkuu wa Hospitali ya Bugando, Profesa Kien Mteta aliishukuru taasisi ya GSM kwa kuamua kulichukua tatizo hilo ambalo ameliita kuwa ni kubwa ukilinganisha na jinsi linavyochukuliwa na jamii ya watanzania.

Dk Kien aliwaambia wanahabari kwamba jumla ya watoto 2000 huzaliwa na vichwa vikubwa katika kanda ya Ziwa peke yake, na mtaalamu wa kuhudumia wagonjwa wa namna hii ni mmoja tu ambapo pia kwa Tanzania nzima, wataalamu wa upasuaji wa watoto wenye vichwa vikubwa wako tisa tu.

Cha kusikitisha ni kwamba kati ya hao, ni wachache sana hurudi kwa ajili ya matibabu bali wengi wao hufariki kwa kufichwa ndani na wazazi wao aidha kwa imani za kishirikina ama kushindwa kwa wazazi kumudu gharama za matibabu.
Mkuu wa Hospitali ya Bugando, Profesa Kien Mteta (kulia) akiongea na wanahabari huku akisikilizwa kwa umakini na Mkurugenzi wa taasisi ya Mifupa na upasuaji Dk Othman Kiloloma (katikati) pamoja na Afisa kutoka GSM, Halfan Kiwamba.
Mtaalamu wa upasuaji wa ubongo na mishipa ya Fahamu, Dk Gerald Mayaya akitoa ufafanuzi kwa wanahabari kuhusiana na kambi ya upasuaji wa watoto wenye vichwa vikubwa katika Hospitali ya Bugando.
Meneja Mkuu wa taasisi ya GSM, Shannon Kiwamba (katikati) akiongea na wanahabari kuhusiana na sera yao mpya ya kusaidia watanzania katika masuala ya elimu na Afya, kulia kwake ni Mkuu wa Hospitali ya Bingando, Prof Kien Mtena na kushoto kwake ni Mkuu wa mawasiliano wa Taasisi ya GSM, Halfan Kiwamba.
Mkuu wa kitenngo cha Upasuaji na Mifupa ambaye ndio mratibu wa kambi ya tiba ya watoto wenye vichwa vikubwa na migongo wazi akifafanua jambo kwa wanahabari(hawapo pichani).
Baadhi ya wahudumu wanaoshiriki kambi ya watoto wenye vichwa vikubwa wakisikiliza viongozi wao wakati wakiongea na wanahabari.
Wanahabari kazini.

Picha ya pamoja ya wawezeshaji wa zoezi la kambi ya upasuaji wa watoto wenye vichwa vikubwa na migongo wazi.
Mkuu wa Hospitali ya Bingando, Prof Kien Mtena (kulia) katika picha ya pamoja na mwanahabari wa Jembe Fm Mwanza G. Sengo.
Taarifa kwa umma kupitia mabango ya Hospitali ya Rufaa Bugando.

No comments:

Post a Comment

Post Top Ad