Health : Kampuni ya Ulinzi ya SGA Yatoa Msaada wa Mashine ya Kupumulia na Mashuka Kwenye Wodi ya Hospitali ya Mwananyamala - Wazalendo 25 Blog

Glory to Story.

PRINTING / GRAPHICS / DESIGN : 0784 643 633

Sunday, 20 December 2015

demo-image

Health : Kampuni ya Ulinzi ya SGA Yatoa Msaada wa Mashine ya Kupumulia na Mashuka Kwenye Wodi ya Hospitali ya Mwananyamala


FILE1910
Mkurugenzi Mkuu wa kampuni ya Ulinzi ya Security Group Africa (SGA), Eric Sambu (kulia) akimkabidhi mshine ya kupumulia na mashuka, Mratibu wa Tiba katika Hospitali ya Mwananyamala, Dk Daniel Nkungu. Makabidhiano hayo yalifanyika mwishoni mwa wiki. Katikati yao ni Meneja Mahusiano kwa wateja wa SGA, Sophia Luhikula.
FILE1941
 Vitu vilivyotolewa msaada Hosipitalini hapo.
FILE1999
Mkurugenzi Mkuu wa kampuni ya Ulinzi ya Security Group Africa (SGA), Eric Sambu (kulia) akimkabidhi mshine ya kupumulia na mashuka, Mratibu wa Tiba katika Hospitali ya Mwananyamala, Dk Daniel Nkungu. Makabidhiano hayo yalifanyika mwishoni mwa wiki. Kushoto ni Meneja Mahusiano kwa wateja wa SGA, Sophia Luhikula.
FILE2071
 Baadhi ya watumishi wa kitengo cha Ambulance cha SGA 
FILE1825
 Mkurugenzi Mkuu wa kampuni ya Ulinzi ya Security Group Africa (SGA), Eric Sambu akizungumza wakati wa kutoa msaada huo.
FILE1801
 Wafanyakazi wa SGA wakibeba msaada huo.
DSC_0032Habari na picha: Father Kidevu Blog

KAMPUNI ya Ulinzi ya Security Group (T) imetoa msaada wa mashine moja ya kupumlia na mashuka 40 kwa wodi ya watoto katika Hospitali ya Mwananyamala, Dar es Salaam

Kampuni ya SGA ilikabidhi mashine hiyo ya kupumulia na mashuka vyote vikiwa na thamani ya Sh milioni tano kwa wodi ya watoto Hospitali ya hapo na kusema hiyo ni kuonyesha jinsi gani wana jali afya za watanzania ambao wanafanyakazi nao.

“Nifuraha yetu kuona familia zetu zipo katika afya njema, lakini pia ulinzi wa mali zetu unaenda vizuri, hivyo leo tumeona tujitoe kidogo kukumbuka jamii yetu hasa watoto ambao ndio taifa la kesho,” alisema Mkurugenzi Mkuu wa SGA, Eric Sambu.

Sambu alisema huo ni muendelezo wa kurejesha kile wanachopata kwa jamii ili kujenga mahusiano mazuri na wataendelea kufanya hivyo kila inapo wezekana.

Akipokea msaada huo, Mratibu wa tiba hospitalini hapo, Dk Daniel Nkungu wanaishukuru kampuni hiyo kuwakumbuka na kuweza kuwasaidia msaada huo ambao kwa kiasi kikubwa utasaidia ufanisi katika utendaji kazi wao na kupunguza vifo vya watoto wachanga.
FILE2104
Picha ya pamoja ilipigwa 
FILE2158
 Wafanyakazi wakiwa wameshika mashuka waliyokabidhi.
FILE2165
 Wafanyakazi wa SGA wakirejesha mashuka hayo katika boxi.
FILE2196
FILE2202
FILE2218
 Baada ya hapo wafanyakazi walishiriki katika tafrija fupi ya kufunga mwaka na kusherehekea mwaka 31 tangu kuanzishwa kwa kampuni hiyo nchini ambapo awali ilijulikana kama Group 4. 
FILE2242
 Mkurugenzi Mkuu wa kampuni ya Ulinzi ya Security Group Africa (SGA), Eric Sambu akizungumza na wafanyakazi wakati wa tafrija.
FILE2278
 Wafanyakazi wakimsikiliza...
FILE2291
 Waliwasikiliza viongozi wao mbalimbali.
FILE2307
 Wakuu mbalimbali wa vitengo walizungumza...
FILE2354
 wafanyakazi walijumuika pamoja na kufurahi.
FILE2406
 Chakula kizuri kiliandaliwa na watu walikula vya kutosha na kupata vinywaji vya kila namna
FILE2420
FILE2427
Watu walikula chakula na kufurahi,

No comments:

Post a Comment

Tuwasiliane

Name

Email *

Message *

Contact Form

Name

Email *

Message *