Siasa Zetu : Nape Ahimiza Mshikamano Mtama, Mkoani Lindi - Wazalendo 25 Blog

Glory to Story.

Friday, 22 May 2015

demo-image

Siasa Zetu : Nape Ahimiza Mshikamano Mtama, Mkoani Lindi


mt1
 Katibu wa Itikadi na Uenezi CCM Taifa akisalimiana na Mzee Masoud Ali Chitende Mbunge Mstaafu wa Jimbo la Mtama mara baada ya kuwasili kwenye kata ya Mtama ambapo alipata nafasi ya kuwasalimu wajumbe wa Halmashauri Kuu za Kata Mtama na Majengo, Mtama mkoani Lindi.
mt2
 Katibu wa Itikadi na Uenezi CCM Taifa Nape Nnauye akiteta jambo na Mwenyekiti wa CCM Kata ya Mtama Mzee Said H. Maluma,kushoto ni Mwenyekiti wa CCM kata ya Majengo Mzee Omari Mataka.
mt4
 Baadhi ya Wajumbe wa Halmashauri Kuu za Kata ya Mtama na Majengo wakimsikiliza Katibu wa Itikadi na Uenezi CCM Taifa Nape Nnauye .
mt5
 Mwenyekiti wa CCM Kata ya Mtama Mzee Said H. Maluma akizungumza jambo wakati wa kumkaribisha Katibu wa NEC Itikadi na Uenezi  CCM Taifa Nape Nnauye kwenye ofisi ya CCM kata ya Mtama.
mt7
 Katibu wa NEC Itikadi na Uenezi Nape Nnauye akizungumza na wajumbe wa Halmashauri Kuu za Kata ya Majengo na Mtama mara baada ya kukutana nao na kuwasalimu kwenye ofisi za CCM kata ya Mtama ambapo aliwataka Wajumbe hao na wana CCM wa Mtama kushikamana na kushirikiana katika kila jambo la kujenga na kuimarisha Chama kwani kufanya hivyo Chama kitakuwa imara zaidi Mtama na kila mwana CCM atajivunia mafanikio ya Chama chake.
mt8
Mkuu wa Wilaya ya Lindi Mheshimiwa Yahaya Nawanda akiteta jambo na Katibu wa NEC Itikadi na Uenezi CCM Taifa Nape Nnauye wakati wa kumsindikiza Katibu wa NEC aliyepita Lindi kwa lengo la kujiandikisha kwenye daftari la kudumu la wapiga kura.

No comments:

Post a Comment

Tuwasiliane

Name

Email *

Message *

Contact Form

Name

Email *

Message *