Matukio: Mhe. Novatus Makunga Awakabidhi Majukumu Viongozi wa Vijiji mbele ya Wananchi - Hai, Kilimanjaro - Wazalendo 25 Blog

Glory to Story.

Habari Mpya

PRINTING / GRAPHICS / DESIGN : 0784 643 633


PRINTING / GRAPHICS / DESIGN : 0676 643 633

5 Feb 2015

Matukio: Mhe. Novatus Makunga Awakabidhi Majukumu Viongozi wa Vijiji mbele ya Wananchi - Hai, Kilimanjaro


Mkuu wa wilaya ya Hai,Novatus Makunga akiwaonyesha wananchi wa kijiji cha Sanya Stesheni Rejesta ya wakazi kama moja ya vitendea kazi vya wenyeviti wa vitongoji.
Mkuu wa wilaya ya Hai,Novatus Makunga akimkabidhi rejesta ya wakazi mmoja ya wenyeviti wa kitongoji katika kijiji cha Sanya Stesheni.
Mmoja ya wazee wa kabila la Wamaasai akimtawaza Mkuu wa wilaya ya Hai,Novatus Makunga kwa miongoni mwa viongozi wa jamii hiyo maarufu kama Laigwanan kwa kumkabidhi rungu.
Mkuu wa wilaya ya Hai Novatus Makunga akiwasalimia wananchi wa kijiji cha Sanya Stesheni baada ya kumkabidhi rungu kama ishara ya uongozi.
Wananchi wa kijiji cha Sanya Stesheni katika mkutano maalumu wa kijiji chao ulioitishwa na mkuu wa wilaya ya Hai,Novatus Makunga kwa lengo la kuwatambulisha rasmi viongozi wapya wa vitongoji na kijiji na kuwakabidhi majukumu yao mbele ya wananchi.
Ofisa mtendaji wa kijiji cha Sanya Stesheni,Edes Mtenga akisoma risala ya wananchi wa kijiji cha Sanya Stesheni kwa mkuu wa wilaya ya Hai,Novatus Makunga.
kaimu Ofisa elimu wilayani Hai,Makarios Mapunda akisisitiza kuanza kwa msako mkali wa kudumu wa watoto wote watoro pamoja na wazazi wasiopeleka watoto shule katika kijiji cha Sanya Stesheni.
Afisa ustawi wa Jamii wilayani Hai Hegla Joseph akisisitiza sheria ya haki ya mtoto ya 2009 ya kuwapeleka watoto shule katika mkutano wa kijiji cha Sanya Stesheni.

No comments:

Post a Comment


PRINTING / GRAPHICS / DESIGN : 0784 643 633