UCHUMI : TANZANIA YAENDELEA KUNUFAIKA NA UHUSIANO MWEMA ULIPO BAINA YAKE NA TAIFA LA CHINA. - Wazalendo 25 Blog

Habari Mpya

Glory to Story.


Post Top Ad


29 Sept 2014

UCHUMI : TANZANIA YAENDELEA KUNUFAIKA NA UHUSIANO MWEMA ULIPO BAINA YAKE NA TAIFA LA CHINA.


 Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu – Uwekezaji na Uwezeshaji Dkk. Mary Nagu akizungumza na waandishi wa Habari wakati wa hafla ya kuadhimisha miaka 65 tangu kuanzishwa Jamhuri ya Watu wa China jana jijini Dar es Salaam.
 : Balozi wa China nchini Tanzania Balozi Lui Youqing akigonga glasi ya mvinyo wakati wa hafla ya kuadhimisha miaka 65 tangu kuanzishwa Jamhuri ya Watu wa China jana jijini Dar es Salaam.
 Picha ya Keki kwa ajili ya hafla ya maadhimisho ya miaka 65 tokea kuanzishwa kwa Jamhuri ya Watu wa China hafla hiyo imefanyika jana jijini Dar es Salaam.
 Balozi wa China nchini Tanzania Balozi Lui Youqing (katikati) akiteta jambo na baadhi ya wageni waalikwa katika hafla ya kuadhimisha miaka 65 tokea kuanzishwa kwa Jamhuri ya Watu wa China jana jijini Dar es Salaam. Kushoto ni Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni Jordan Rugimbana na Afisa anayeshughulikia masuala ya Menejimenti na Programu wa Aga Khana Development Network Bw. Navroz Lakhani
 Baadhi ya wageni wakisoma vitabu wakati wa hafla ya kuadhimisha miaka 65 tangu kuanzishwa kwa Jamhuri ya Watu wa China jana jijini Dar es Salaam.Picha na Frank Shija, WHVUM.
========  ========  =======
Tanzania yaendelea kunufaika na uhusiano mwema ulipo baina yake na Taifa la China.

Na; Daud Manongi,    WHVUM.

Hadi kufikia mwishoni mwa mwaka 2013 China imetoa msaada wa zaidi ya dola za Kimarekani bilioni 1.943 kwa ajili ya kusaidia miradi mbalimbali ya maendeleo nchini Tanzania, ushirikiano wa kibiashara  dola bilioni 3.7 na uwekezaji dola bilioni 2.5 na jumla ya makampuni 500 yamewekeza nchini Tanzania.

Haya yamebainishwa na Waziri wa Nci ofisi ya Waziri Mkuu – Uwekezaji na Uwezeshaji Dkt. Mary Nagu aliyekuwa mgeni rasmi katika hafla ya miaka 65 ya toka kuanzishwa kwa Jamhuri ya Watu wa China jana jijini Dar es Salaam.

Dkt Nagu amesema kuwa msaada huo utasaidia katika kutekeleza miradi ya maendeleo ikiwema Bandari ya Bagamoyo, mradi wa EPZ, usambazaji wa umeme ukanda wa Kaskazini – Mashariki, Elimu kwa njia ya mtandao,Serikali Mtandao kwa ajili ya Zanzibar na Umeme wa upepo katika mkoa wa Singida. Aliongeza kuwa kukamilika kwa miradi hiyo kutafungua njia za uchumi na kusababisha Tanzania kuwa na uchumi imara na endelevu.

“Najisikia faraja kusema kuwama pamoja na mafanikia chanya tunayopata Tanzania bado ina miradi mingi ambayo inahitaji msaada wa kifedha na kitaalam kutoka kwa Jamhuri ya Watu wa China na ni imani kuwa wataendelea kutoa ushirikiano katika kufanikisha miradi hiyo” Alisema Dkt. Nagu.

Kwa upande wake Balozi wa China hapa nchini Balozi Lui Youqing amesema kuwa nchi yake itaendelea kuisaidi Tanzania kwa kuwa kumekuwa na mahusiano mazuri nay a muda mrefu baina ya nchi hizi mbili.

Balozi Youqing ameongeza kuwa Tanzania inavutia wakezaji kwa kuwa na mazingira salama ya kisiasa na kijamii ambapo anashawishika kuunganisha wawekezaji wa China kushirikiana na wawekezaji wengine katika kupunguza umasikini na kuleta maendeleo akitolea mfano ushirikiano katika sekta ya majengo.

“Tanzania ni nchi kubwa yenye maono na inayovutia zaidi kimataifa kutokana na uimara wake katika Nyanja za siasa na uchumi jamii, imekuwa na ushawishi wa hali ya juu katika anga za kikanda na kimataifa, hali inafanya wawekezaji kutoka sehemu kama EU, US, Japana na kwingineko waongeze uwekezaji, ata mimi binafsi nashawishika kuwashawishi wawekezaji wa China kuwekeza zaidi katika nchi hii” Alisema Balozi Youqing.

China inasherehekea miaka 65 toke kuanzishwa kwake mnamo mwaka 1949, wkati huo huo ni miaka 50 sasa tokea Taifa kuanzisha mahusiano ya kidiplomasia kati yake na Tanzania uhusiano ambao umeasisiwa na Hayati Baba wa Taifa Mwalimu Julius Kambarage Nyerere na Hayati Mao Zedong.

No comments:

Post a Comment

Post Top Ad