UPDATES ZA MSIBA :MSIBA WA GEORGE TYSON, SASA KUAGWA VIWANJA VYA LEADERS JUMATANO NA KUSAFIRISHWA KWENDA NAIROBI, KENYA - Wazalendo 25 Blog

Glory to Story.

Habari Mpya

PRINTING / GRAPHICS / DESIGN : 0784 643 633


PRINTING / GRAPHICS / DESIGN : 0676 643 633

Tuesday 3 June 2014

UPDATES ZA MSIBA :MSIBA WA GEORGE TYSON, SASA KUAGWA VIWANJA VYA LEADERS JUMATANO NA KUSAFIRISHWA KWENDA NAIROBI, KENYA


Mwili wa Marehemu George Tyson (pichani) utapelekwa nyumbani kwa marehemu Mbezi Beach (eneo la Makonde) jijini Dar es salaam leo Jumanne Juni 3, 2014  kuanzia majira ya saa kumi jioni kwa ajili ya kuaga. 
Mwili utakuwepo nyumbani hapo mpaka siku ya Jumatano Juni 4, 2014 ambapo mwili utapelekwa kwenye viwanya vya Leaders Club, Kinondoni, jijini Dar es salaam,  kwa ajili ya shughuli ya kuaga mwili na ibada fupi.
Baadae mwili utapelekwa kwenye Uwanja wa ndege wa Mwalimu J.K.Nyerere tayari kwa kusafirishwa kwenye jijini Nairobi nchini Kenya kwa mazishi.
Tutaendelea kuwaletea taarifa 
kadri zitakavyokuwa zikitufikia.

No comments:

Post a Comment