PONGEZI: DKT. SHEIN AWAPONGEZA WAFANYAKAZI WA WIZARA ZILIZO CHINI YA OFISI YA RAIS NA MWENYEKITI WA BARAZA LA MAPINDUZI - Wazalendo 25 Blog

Glory to Story.

Habari Mpya

PRINTING / GRAPHICS / DESIGN : 0784 643 633


PRINTING / GRAPHICS / DESIGN : 0676 643 633

Wednesday 4 June 2014

PONGEZI: DKT. SHEIN AWAPONGEZA WAFANYAKAZI WA WIZARA ZILIZO CHINI YA OFISI YA RAIS NA MWENYEKITI WA BARAZA LA MAPINDUZI



 Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dkt.Ali Mohamed Shein akizungumza na wafanyakazi wa Wizara zilizo chini ya Ofisi ya Rais na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi baada ya kulanao pamoja chakula katika fahla ya kuwapongeza wafanyakazi hao baada ya  kupitishwa bajeti za Wizara hizo katika kikao cha Baraza la Wawakilishi kinachoendelea ,hafla hiyo ilifanyika leo viwanja vya Ikulu,(wapili kulia)Makamo wa Pili wa Rais Balozi Seif Ali Iddi,akifuatiwa na Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Idara maalum za SMZ Haji Omar Kheri
 Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dkt. Ali Mohamed Shein (wa pili kushoto) Makamo wa Pili wa Rais Balozi Seif Ali Iddi,(kushoto) Katibu Mkuu Kiongozi Dkt.Abulhamid Yahya Mzee,(kulia) na Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Ikulu na Utawala BoraDkt.Mwinyihaji Makame Mwadini (wapili kulia) wakiwapongeza wafanyakazi mbali mbali wa Wizara zilizo chini ya Ofisi ya Rais na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi katika hafla ya chakula iliyofanyika  baada ya kupitishwa bajeti za Wizara hizo katika kikao cha Baraza la Wawakilishi. Hafla hiyo ilifanyika viwanja vya Ikulu, Zanzibar
 Baadhi ya Viongozi wa Wizara mbali mbali  zilizo chini ya Ofisi ya Rais na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi wakiwa katika  hafla ya chakula iliyofanyika  baada ya kupitishwa bajeti za Wizara hizo katika kikao cha Baraza la Wawakilishi kinachoendelea. Hafla hiyo ilifanyika  viwanja vya Ikulu
Baadhi ya watendaji na washauri wa Ofisi ya Rais Ikulu  wakiwa katika  hafla ya chakula iliyofanyika  baada ya kupitishwa bajeti za Wizara zilizo chini ya Ofisi ya Rais na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi katika kikao cha Baraza la Wawakilishi kinachoendelea. 
Picha na Ramadhan Othman,Ikulu

No comments:

Post a Comment