KUTOKA KENYA : RAILA ASEMA LAZIMA CORD WATUE ELDORET NA NAROK, POLISI WAMEZUIA MIKUTANO YA KISIASA - Wazalendo 25 Blog

Habari Mpya

Glory to Story.


Post Top Ad


25 Jun 2014

KUTOKA KENYA : RAILA ASEMA LAZIMA CORD WATUE ELDORET NA NAROK, POLISI WAMEZUIA MIKUTANO YA KISIASA


Raila Odinga (kushoto) na Moses Wetangula
Viongozi wa CORD Raila Odinga (kushoto) na Moses Wetangula wakihutubia wanahabari Juni 3, 2014 jijini Nairobi. Picha/EVNAS HABIL. 


Na VALENTINE OBARA
 
Viongozi wa Muungano wa Cord wameapa kuendelea na mikutano iliyopangwa kufanyika Eldoret na Narok licha ya polisi kusema hakuna usalama wa kutosha kuandaa mikutano ya kisiasa.

VIONGOZI wa muungano wa Cord wameapa kuendelea na mikutano iliyopangwa kufanyika Eldoret na Narok licha ya polisi kusema hakuna usalama wa kutosha kuandaa mikutano ya kisiasa.
Kinara wa muungano huo Bw Raila Odinga amesema hawajapokea ripoti yoyote kuhusu ukosefu wa usalama Eldoret, na hivyo basi hawatatii agizo lililotolewa na Gavana Jackson Mandago pamoja na kamati ya usalama katika kaunti hiyo.
“Hatujajua kama kuna hali ya hatari kule Eldoret…haijatangazwa kwa hivyo sisi hatujui. Natangaza hapa kwamba tutaenda Eldoret wapende wasipende, na vile vile tutaenda kule Ntulele na tunatarajia kupewa ulinzi inavyohitajika,” akasema Bw Odinga.
Kulingana naye, ni kinaya kuwa polisi wanasema hakuna usalama ilhali ni jukumu lao kutoa ulinzi kwa wananchi wanaohudhuria mikutano kama hiyo.
“Polisi wana jukumu la kulinda wananchi kwa mikutano. Katiba inasema tu wanafaa kupewa notisi ili walinde wananchi katika mikutano,” akasema.
Mkutano wa Eldoret ulipangiwa kufanyika Ijumaa huku ule wa Narok ukitarajiwa kuandaliwa Ntulele Jumamosi. Chanzo Taifa Leo

No comments:

Post a Comment

Post Top Ad