"Nimeshinda kesi tena! Kwa kweli Mungu anatupenda sana na tutaendelea kupambana kutafuta haki bila hofu. Miili yetu na nafsi zetu zimepoteza maumivu kwa sababu ya mateso yaliyojaa uongi na hila. Hata hivyo tutaendelea na kelele za kupigania haki bila kurudi nyuma huku uvumilivu ukiwa nguzo yetu kuu" alisema Mbunge Lema , katika viwanja vya Mahakama Kuu Arusha mara baada ya kushinda kesi dhidi yake na Mkuu wa Mkoa wa Arusha, Magesa Mulongo zikihusisha kilichodaiwa kuwa uchochezi kwa wanafunzi wa Uhasibu Arusha wamzomee Mulongo na kufanya fujo... Kesi hiyo imefutiliwa mbali baada ya washitaki kuomba hivyo pamoja na kwamba leo ndio ilikuwa siku ya kuanza kusikiliza ushahidi wa Mkuu wa Mkoa, Dean of Students, Makamu Mkuu wa Chuo na Maofisa wa Polisi wakiongozwa na OCD Muroto. Kwa hisani ya Seria Tumainiel (SeriaMtoto WikiLiks Tumainiel) |
NISHATI SAFI INAMUONDOLEA ADHA MTOTO WA KIKE - KIJAJI
-
*Waziri wa Nchi, Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira) Mhe. Dkt.
Ashatu Kijaji amesema uwepo wa Nishati Safi ya Kupikia kunamuokoa mtoto
kike ...
49 minutes ago
No comments:
Post a Comment