DIAMOND PLATNUMZ AMZAWADIA GARI MUHIDIN GURUMO - Wazalendo 25 Blog

Habari Mpya

Glory to Story.


Post Top Ad


30 Aug 2013

DIAMOND PLATNUMZ AMZAWADIA GARI MUHIDIN GURUMO

1Mwanamuziki Diamond Platnum akimkabidhi funguo ya gari aina ya Toyota Funcargo mwanamuziki mkongwe nchini mzee Muhidin Gurumo kama zawadi yake kwa mkongwe huyo wa muziki baada ya kustaafu rasmi kuimba muziki, Diamond alitoa zawadi hiyo kwa Gurumo katika hafla yake ya uzinduzi wa video yake mpya ya wimbo Nomber One aliyoirekodi huko Afrika Kusini ikigharimu kiasi cha dola elfu 30.000 zaidi ya milioni arobaini za Tanzania, Video hiyo imetengenezwa kwa viwango vya kimataifa na itaweza kumtangaza vyema kijana huyo wa kitanzania katika ulimwengu wa muziki hasa kimataifa, Hafla hiyo imefanyika kwenye hoteli ya Serena Dar es salaam na imehudhuriwa na wasanii pamoja na waigizaji wa filamu na watu maarufu mbalimbali  2Mzee  Muhidin Gurumo akimshukuru Diamond kwa kumzawadia gari jambo ambalo kwake ni kama ndoto kwakuwa amestaafu akiwa hana usafiri “Yaani sijui hata mke wangu nikimwambia atanielewaje manake ni jambo la kushangaza kwangu” Alisema mzee Gurumo 3Diamond akimuongoza mzee Gurumo kwenda kumuonyesha gari 5Diamond akimuonyesha Mzee Gurumo gari 6Akimuelekeza jambo baada ya mzee Gurumo kuingia kwenye gari 7 
Diamond akizungumza machache kushukuru mashabiki wake na watu mbalimbali waliomsaidia kufikia hapo alipo 9Diamond na madansa wake wakitumbuiza katika hafla hiyo 10Wasanii mbalimbali pamoja na MaDJ walikuwepo katika hafla hiyo hapa ni Dully Sykes na MawanaFA wakiwa na baadhi ya MaDJ 11Maurice Njowoka kutoka Cocacola wa pili kutoka kushoto na Mwanamuziki AY wa tatu kutoka kushoto pamoja na wadau wengine wakiwa katika hafla hiyo 12 
Mwigizaji Jaquiline Wolper naye alitia timu  13Mkurugenzi wa ASET Asha Baraka akiwa na mama yake Diamond Wadau mbalimbali wakiwa katika hafla hiyo 16 17Mzee Gurumo akihojiwa na waandishi wa habari 18Hawa marafiki zangu wakakumbushia miaka kadhaa waliyofunga ndoa kwa kulishana mishikaki ilipendeza katikati ni Nancy Sumari akishuhudia 19Kulia ni Irene Uwoya kushoto Salma Msangi  20Kushoto AY na Salama Jabir wakipiga story na wadau mbalimbali 21 22Kutoka kulia ni Raymond Kigosi, Irene Uwoya na JB wakiwa katika hafla hiyo.Picha Na Fullshangwe Blog

No comments:

Post a Comment

Post Top Ad