Waandishi wa Habari 'Bloggers' kutoka Tanzania Bloggers Network (TBN) ambao wameshiriki kikamilifu kwenye Kamati ya maandalizi ya mkutano huo wakiwa kwenye picha ya pamoja.
Baadhi ya waandishi wa habari wameelezea kuridhishwa na hatua ambazo serikali imekuwa ikichukua katika kuimarisha sekta ya habari.
Msemaji Mkuu wa Serikali, Greyson Msigwa, amewashauri waandishi wa habari kuwa, kupitia Mkutano huu, wanapaswa kuzingatia weledi katika taaluma yao hasa kuelekea Uchaguzi Mkuu ili kulinda usalama wa taifa.
Makamu Mwenyekiti wa Kamati ya Maudhui, Saida Muki, amesisitiza kuwa waandishi wa habari wanapaswa kuwa makini na matumizi ya Teknolojia ya Akili Bandia (AI) wakati huu wa kuelekea Uchaguzi Mkuu ili wasiwasilishe maudhui yanayoweza kupotosha umma.
Mkuu wa Mkoa wa Dodoma Rosemary Senyamule amewakaribisha Waandishi wa Habari Jijini Dodoma na kuwata watembelee maeneo mbalimbali ambayo yamejengwa majengo ya kisasa na kusema kuwa Dodoma inaendelea kukua kiuchumi na kuleta chachu ya maendeleo kila uchao.
No comments:
Post a Comment