SUDAN WANAFANYA TAMASHA LA VIAZI - Wazalendo 25 Blog

Glory to Story.

Habari Mpya

PRINTING / GRAPHICS / DESIGN : 0784 643 633


PRINTING / GRAPHICS / DESIGN : 0676 643 633

13 Dec 2012

SUDAN WANAFANYA TAMASHA LA VIAZI


Msichana mdogo akiwa amebeba ndoo ya viazi akiwa na kakake mdogo nchini Sudan

Tamasha la viazi linafanyika katika mji mkuu wa Sudan , Khartoum, kwa lengo la kuwahamasisha watu kula na kulima zaidi viazi .
Maharagwe, wali , mihogo na nafaka nyingine vimekuwa vyakula vikuu zaidi kuliko viazi nchini Sudan na maeneo mengine ya Afrika
Zaidi ya vyakula sitini vilivyoandaliwa kwa viazi vitaandaliwa katika tamasha hilo kuwawezesha watu kuonja.
Kutakuwa pia na maonyesho ya mbinu za ukulima wa viazi na namna ya kuvihifadhi .
Waandalizi wa mkutano huo wanasema kuwa Sudan inaweza kuwa mzalishaji mkuu wa viazi barani Afrika kutokana na hali yake ya hewa na raslimali kubwa ya ardhi.
Chanzo: BBC Swahili

No comments:

Post a Comment


PRINTING / GRAPHICS / DESIGN : 0784 643 633