HOTELI YA GIRAFFE VIEW YAFUNGIWA KUTOKANA NA UCHAFUZI WA MAZINGIRA - Wazalendo 25 Blog

Glory to Story.

Habari Mpya

PRINTING / GRAPHICS / DESIGN : 0784 643 633


PRINTING / GRAPHICS / DESIGN : 0676 643 633

20 Dec 2012

HOTELI YA GIRAFFE VIEW YAFUNGIWA KUTOKANA NA UCHAFUZI WA MAZINGIRA

Hoteli ya Girafee Ocen View iliofungiwa na Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais Terezya Huvisa wakati alipotembelea leo katika mfululizo wa ziara ya kukagua hali ya Mazingira kwenye fukwe za Bahari.
Uchafu katika Ufukwe wa Hoteli ya Girafee Ocen View.

Lulu Mussa na Ali Meja - Ofisi ya Makamu wa Rais

Waziri wa Nchi wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais – Mazingira Dk. Terezya Huvisa hii leo ameendelea na ziara ya kikazi ya kukagua hali ya mazingira katika hoteli zilizopo pembezoni mwa fuke za bahari ya hindi, jijini Dar es Salaam.

Ziara ya leo imeanzia katika hotel ya Giraffe Ocean View, na katika hali ya kushangaza maagizo aliyotoa Naibu Waziri Charles Kitwanga katika hoteli hiyo mapema mwezi huu ya kurekebisha mfumo wa majitaka na kuweka fukwe katika hali ya usafi hayajazingatiwa.

Hatua kali zimechukuwa wa Hotel hiyo ikiwa ni pamoja na kufungiwa mpaka hapo itakapotimiza masharti yaliyowekwa kwa mujibu wa sheria ya mazingira ya mwaka 2004. “Naifunga Hotel hii ya Girafee mpaka hapo itakapotimiza masharti ya hifadhi ya mazingira” alilisitiza Dkt. Huvisa.

Sambamba na hilo Waziri Huvisa ameipongeza Hotel ya Beach Comber kwa kuwa na mkakati endelevu wa mfumo wa maji taka na hifadhi ya fukwe kwa ujumla. Dkt. Huvisa amesema kuwa zoezi hilo ni mkakati endelevu wa kukagua hoteli zote na viwanda, Ofisi ya Makamu wa Rais – Idara ya Mazingira kwa kushirikiana na Baraza la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC) wanafanya kazi hiyo kwa kikamilifu.

Kwa mujibu wa sheria ya Mazingira ya mwaka 2004, Hoteli na Viwanda vyote vilivyoanzishwa kabla ya matumizi ya sheria hiyo vinatakiwa kufanya (Environmental Audit) na baada ya sheria ya Mazingira hutakiwa kufanya Tathmini ya Athari za Mazingira (Environmental Impact Assessment).

Katika ziara ya siku mbili iliyofanywa na Waziri Huvisa pamoja na Naibu wake Charles Kitwanga imepelekea kuchukua hatua kali za kisheria ambapo Hotel ya Double Tree na Giraffe Ocean View zimefungiwa mpaka hapo zitakotimiza masharti waliyopewa.

No comments:

Post a Comment


PRINTING / GRAPHICS / DESIGN : 0784 643 633